Welcome to our online store Portal

Template Information

Saturday, December 28, 2013

TUGHE HALI YAZIDI KUA TETE

http://www.azizicompdoc.blogspot.com/
Hali si shwari katika Chama cha Wafanyakazi wa Afya na Serikali Kuu (Tughe), baada ya Baraza lake Kuu la Taifa kuwasimamisha viongozi wakuu hadi mkutano mkuu wa chama hicho utakapoitishwa.
Viongozi hao wamesimamishwa kutokana na kukacha mkutano wa Baraza Kuu la Taifa baada ya kuhojiwa kwa tuhuma za ubadhirifu na kuvunja katiba.
Mwenyekiti wa Kamati Teule, Archie Mntambo alisema viongozi hao walikimbia baada ya kuhojiwa juu ya uvunjifu wa katiba kwa kutoitisha vikao vya baraza hilo na ubadhirifu wa fedha za chama hicho.
Akizungumza kabla ya kuahirisha mkutano huo mwishoni mwa wiki iliyopita mjini hapa, Mntambo aliwataja waliosimamishwa kuwa ni Mwenyekiti wa Taifa, Dk Diwani Mrutu, Makamu Mwenyekiti, Maclean Chitete na Katibu Mkuu Ally Kiwenge.
Alisema kikao hicho hakina madaraka ya kuwavua uongozi na kwamba suala hilo litapelekwa kwenye mkutano mkuu wenye uamuzi wa mwisho kuhusiana na jambo hilo.
“Tangu wachaguliwe Septemba, 2011, hawajawahi kuitisha kikao cha Baraza Kuu la Taifa ambalo ndilo linalohusika na upangaji wa bajeti ya chama,” alisema.
Alisema viongozi hao baada ya kusomewa mashtaka yao waliitwa mmojammoja mbele ya wajumbe wa baraza hilo na kuhojiwa lakini kabla ya kupewa majibu ya tuhuma zao waliondoka.
Katiba ya chama hicho inautaka uongozi kuitisha vikao vya baraza kuu mara mbili kwa kila mwaka.

Hata hivyo, Chitete alikana kusimamishwa akisema mkutano huo ambao ulianza Desemba 19 mwaka huu, ulimalizika kwa mwenyekiti kuufunga... “Mwenyekiti wa Taifa alifunga kikao na mimi nikaondoka kwenda hotelini kwangu.”
Kwa upande wake, Dk Mrutu alisema jana kuwa kikao hicho kilichochagua kamati teule hakikuwa halali kwa sababu alifunga kikao bila uamuzi huo kufikiwa.
Kuhusu tuhuma za ubadhirifu na uvunjaji wa katiba, alikataa kulizungumzia suala hilo kwa undani na kusema anasubiri barua ya kumtuhumu kutoka katika kikao halali cha chama.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop