Welcome to our online store Portal

Template Information

Friday, January 17, 2014

MAITI YAPORWA KANISANI MBEYA

http://azizicompdoc.blogspot.com/
Kundi la vijana 60, juzi walipora mwili wa marehemu Gabriel Ngalele ukiwa unaombewa kwenye Kanisa la Tanzania Assemblies Of God (TAG) eneo la Uyole jijini baada ya kuchoshwa na ibada ndefu ya mchungaji.
Ibada hiyo ilikuwa ikiendeshwa na Mchungaji, Edward Mtweve wa kanisa hilo ambaye alijikuta kwenye mazingira magumu baada ya vijana hao wanaodaiwa kuwa ni madereva wa pikipiki kuvamia madhabahu na kubeba sanduku lililokuwa na mwili wa marehemu.
Marehemu Ngatele alikuwa dereva wa pikipiki na alifariki kwenye ajali iliyotokea eneo la Sae baada ya pikipiki yake kuligonga lori lililoharibika katikati ya barabara. Katika ajali hiyo, abiria pia alifariki.
Mwili wa marehemu ulipelekwa katika kanisa hilo, na wakati mchungaji akiendesha ibada kulijitokeza kelele za hapa na pale na kusababisha mchungaji kuomba utulivu mara kadhaa.
Lakini kelele nyingi zililipuka ghafla zikiwamo za kulalamika kwamba ibada ilikuwa ndefu na hatimaye vijana wengi walionekana wakiingia kwenye mlango na kuvamia madhabahu na kutoka na mwili wa marehemu.
Baada ya kuuchukua mwili, vijana hao walikwenda kwenye makaburi kuuzika wakati naye mchungaji akiendelea kuhubiri waumini waliobaki ndani ya kanisa.
Mchungaji Mtweve alilazimika kwenda nyumbani baada ya kumaliza ibada badala ya makaburini, huku vijana nao wakiendelea na taratibu za mazishi kwa utaratibu uliosimamiwa na Mwenyekiti wa waendesha pikipiki Mbeya, Vicent Mwashoma.
Mwendesha pikipiki aliyetajwa kwa jina la Bahati Mwasote alilazimika kuendesha ibada ya mazishi.
Mchungaji Edward Mtweve alipoulizwa kuhusu tukio hilo alisema alisikitishwa na kitendo cha kuvurugwa kwa ibada.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop