Welcome to our online store Portal

Template Information

Friday, January 17, 2014

POLISI WADAIWA KUUA

http://azizicompdoc.blogspot.com/
Polisi wilayani Kaliua, inadaiwa kumuua mtu mmoja na kumjeruhi mwingine baada ya wananchi zaidi ya 200 kuvamia kituo kidogo cha polisi kwa lengo la kumtoa mtuhumiwa ili wajichukulie sheria mkononi.
Tukio hilo limetokea baada ya wananchi wa Kijiji cha King’wangoko, Kata ya Sasu kuvamia kutaka kumdhuru Shija Matenga, anayetuhumiwa kuiba ng’ombe watano Kasulu, Kigoma.
Kamanda wa Polisi mkoani Tabora, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Peter Ouma, akielezea tukio hilo alisema Mkuu wa Kituo Kidogo cha King’wangoko, Sajenti Kimola alipokea simu kutoka kwa Wakala wa Mnada wa Konanne, kuwa wananchi wamemkamata na wanataka kumuua.
Kutokana na hali hiyo, Sajenti Kimola alituma askari wawili wakiwa na silaha na kumwokoa mtuhumiwa na kuanza kuondoka naye kitendo kilichokasirikiwa na wananchi walioanza kurusha mawe na fimbo ili kuwazuia askari wasimpeleke kituoni hali hiyo ilichosababisha askari kupiga risasi hewani kuwatawanya wananchi.
“Askari walitumwa walifanikiwa kumwokoa mtuhumiwa jambo ambalo liliwachukiza wananchi waliotupa mawe na fimbo ili kuwazuia askari wasiondoke na mtuhumiwa ambao walilazimika kufyatua risasi hewani kuwatawanya,”alisema Ouma.
Kwa mujibu wa Kamanda Ouma, baada ya askari kumfikisha mtuhumiwa kituoni na kumfungia mahabusu, wananchi walifuatilia na kufika kituoni alipo mtuhumiwa na kushinikiza atolewe.
Alisema askari walipoona wananchi wanataka kutumia nguvu walifyatua risasi hewani kuwatawanya na bahati mbaya risasi moja ilimpata John Joseph bega la kulia kufariki papohapo.
Mwingine aitwaye Malembeka Matemele alijeruhiwa kwenye paja la mguu wa kulia na amelazwa Hospitali ya Wilaya ya Urambo. kwa matibabu.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop