Chuo
Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimehadharisha walaji wa nyama ya
nguruwe nchini, kuwa wanakabiliwa na hatari ya kupata kifafa.
Utafiti
wa kisayansi uliofanywa na SUA, umebaini kuwa baadhi ya nguruwe wana
minyoo aina ya tegu ambao nyama yao ikiliwa bila kuiva vizuri, mlaji
atapata minyoo hiyo ambayo huingia kichwani na kusababisha kifafa.
Akizungumza
na mwandishi hivi karibuni, Mhadhiri na Mtafiti wa Idara ya Sayansi ya
Wanyama na Uzalishaji ya SUA, Profesa Faustine Lekule, alisema sampuli
za utafiti huo kutoka Mbeya, zimebaini nguruwe wengi wakiwamo
wanaosafirishwa katika miji mikubwa wameathirika na minyoo hiyo.
Kwa
mujibu wa Profesa Lekule, wataalamu wa SUA wanaosimamia Mradi wa
Utafiti wa Kuboresha Ufugaji wa nguruwe kwa mkoa wa Mbeya ili kuinua
pato la kaya, unaofadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Maendeleo la
Denmark (DANIDA), walibaini hatari hiyo baada ya kuchukua sampuli ya
nyama ya nguruwe kwa ajili ya vipimo.
“Majibu
ya sampuli ambazo wataalamu wamezichukua kutoka kwa nguruwe wa wafugaji
kwenye baadhi ya vijiji, wamebainika kukumbwa na hatari hii.
“Lazima
jitihada za makusudi zichukuliwe katika kutafuta ufumbuzi wa pamoja wa
tatizo hili kati ya watafiti na Serikali,” alisema Profesa Lekule.
Alisema
maambukizi ya tegu au minyoo ya nguruwe yanatokana na tabia za baadhi
ya wafugaji kutozingatia ufugaji bora kwa kuwaacha kujitafutia chakula
na maji mitaani na kula kinyesi cha binadamu.
Kwa
mujibu wa Profesa Lekule, baadhi ya wafugaji wamekuwa wakijisaidia
vichakani na kuwaacha nguruwe kutafuta malisho katika vichaka na kula
kinyesi chao, hali inayochangia ongezeko la maambukizi ya minyoo ya tegu
hao.
Baada
ya kula kinyesi minyoo humwingia mwilini na kumdhoofisha na baadaye
binadamu anapokula nyama ambayo haijaiva vizuri, minyoo hiyo humwingia
na kusababisha kifafa baada ya kuingia kichwani.
Alisema
athari za kuenea kwa maambuziki hayo inaweza kutokea katika miji
mikubwa ikiwamo Dar es Salaam kwa kuwa nguruwe wa Mbeya husafirishwa na
kuuzwa maeneo hayo.
“Hatua
hii inaweza kusababisha kusambaa kwa ugonjwa huu, hivyo ushirikiano
kati ya wafugaji, wafanyabiashara, Serikali na wataalamu wa afya katika
kufikia hatua ya kumaliza changamoto hii unahitajika,” alibainisha
Profesa Lekule.
0 comments:
Post a Comment