Mshindi
wa shilingi milioni 10 katika promosheni ya Tigo ‘Shinda Kitita na Tigo
Pesa’ Bi. Margaret Mbungu Mwanjala akifurahia zawadi ya kitita cha
fedha alizokabidhiwa na Mratibu wa Promosheni wa Tigo Pesa Bi. Mary
Rutta (kulia) mapema leo jijini Dar es Salaam. Mpaka sasa wateja 1,590
wameweza kujishindia zawadi ya fedha taslimu milioni 560 huku milioni
560 zingine zikibakia kushindaniwa katika wiki tatu zijazo.
Mshindi
wa shilingi milioni mbili katika promosheni ya Tigo ‘Shinda Kitita na
Tigo Pesa’ Bw. Emmanuel William Mabojola (kushoto) akihesabu pesa
alizojishindia kwenye shindano hilo mapema leo jijini Dar es
Salaam. Akishuhudia ni Mratibu wa Promosheni wa Tigo Pesa Bi. Mary
Rutta.
Bi.
Vaileth Methusela Mkuku naye akihesabu shilingi milioni mbili
alizoshinda kutoka Tigo. Zawadi zinazoshindaniwa ni za shilingi
200,000/- kwa wateja 50 kila siku, milioni 2 kwa wateja 20 kila wiki na
zawadi ya juu kabisa ni ya fedha taslimu milioni 10 wanayoshinda wateja
watano kila baada ya wiki mbili.
Mratibu
wa Promosheni wa Tigo Pesa Bi. Mary Rutta (kulia) akimpongeza mshindi
wa shilingi milioni mbili katika promosheni ya ‘Shinda Kitita na Tigo
Pesa’ Bw. Boniface Bembele Mwita aliyekabidhiwa kitita chake mapema leo
jijini Dar es Salaam. Kushiriki katika promosheni hii mteja wa Tigo
anatakiwa kutumia akaunti yake ya Tigo Pesa kutuma fedha, kununua
bidhaa, kuongeza salio na kulipia bili za huduma mbali mbali.
Ikiwa
ni mwezi tu tangu promosheni ya Tigo ‘Cheza Kwa Furaha Unaposhinda
Kitita na Tigo Pesa’ ilipozinduliwa, wateja 1,590 wameweza kujishindia
zawadi ya fedha taslimu milioni 560 huku milioni 560 zingine zikibakia
kushindaniwa katika wiki tatu zijazo.
Akizungumzia
muenendo wa promosheni hiyo katika makao makuu ya kampuni hiyo ya simu
leo jijini Dar es Salaam, Mratibu wa Promosheni wa Tigo Pesa Mary Rutta
amesema kwamba zawadi zilizoshindaniwa ni za shilingi 200,000/- kwa
wateja 50 kila siku, milioni 2 kwa wateja 20 kila wiki na zawadi ya juu
kabisa ni ya fedha taslimu milioni 10 wanayoshinda wateja watano kila
baada ya wiki mbili.
“Tunazidi
kushuhudia wateja wengi zaidi wakifurahia kushinda hizi zawadi za fedha
taslimu kwa kufanya miamala kupitia akaunti zao za Tigo Pesa. Hii ni
pamoja na kutuma fedha, kununua bidhaa, kuongeza salio au kulipia bili
mbali mbali. Tunafuraha kwamba washindi wametoka mikoa yote nchini na
kumekuwa na uwiano mzuri baina ya washindi kutoka mijini na vijijini,”
alisema Rutta.
Mratibu
huyo wa promosheni aliendelea kutoa wito kwa wateja wa Tigo kuendelea
kufanya miamala ya Tigo Pesa akisisitiza kwamba zimesalia wiki tatu tu
promosheni hii kuisha katikati ya mwezi Februari.
“Promosheni
yetu inadhihirisha kwamba Tigo ni kampuni ambayo inaendelea kuweka
jitihada ya kila siku katika kukidhi matarajio ya wateja wake. Tunaamini
kuwa promosheni hii kwa namna moja au nyingine imeweza kubadilisha
maisha ya washindi hawa 1,590 ambao wengi wao waliweza kupatiwa pesa zao
wakati wa msimu wa Krismasi na Mwaka Mpya, muda ambao mahitaji ya
kifedha huwa juu,” alisema.
Mkutano
huu wa waandishi wa habari pia umehudhuriwa na washindi watano kati ya
washindi 375 wa wiki iliyopita ambao walielezea promosheni hii kwamba ni
“ya kweli” na yenye “kufurahisha.” Washindi waliokuwepo wale
walioshinda shilingi milioni mbili waliwemo Emmanuel William Mabojola,
Boniface Bembele Mwita, Violeth Msela Mkuku and Amina Saida Aboud.
Mwingine ni Margaret Mbungu Mwanjala aliyeshinda shilingi milioni 10.
“Ni
kwa neema ya Mungu nimeweza kushinda hizi fedha. Hakika imekuja kwa
kunistukiza, sikutarajia na sikuamini kabisa,” alisema Mwanjala
aliyeshinda zawadi hiyo nono ya juu kabisa.
Ili
kupata nafasi ya kushinda katika muda uliobaki wa promosheni hii, Rutta
aliwasihi wateja wa Tigo “kuendelea kutumia akaunti zao za Tigo Pesa
kwa ajili ya kutuma fedha, kununua bidhaa, kuongeza salio au kulipia
bili mbali mbali, ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kushinda.”
0 comments:
Post a Comment