Welcome to our online store Portal

Template Information

Saturday, February 15, 2014

BAKRESA AZIDI KUPANUA HUDUMA ZAKE NDANI NA NJE YA AFRIKA MASHARIKI


 
 Unapozungumzia uchumi na uwekezaji katika Tanzania huwezi kuiweka kando Bakhresa Group of Companies, kampuni inayomilikiwa na mfanyabiashara mzalendo Said Salim Bhakresa.
Siyo uchumi na uwekezaji pekee, bali kampuni hiyo pia ni soko la ajira kwa Watanzania wenye utaalamu katika fani mbalimbali, hata wale wasio wataalamu ambao hufanya kazi kwa muda na kupata ujira wao unaowawezesha kuendesha maisha ya kila siku.
Kimuundo Azam Bakhresa Group Companies inajumuisha kampuni mbalimbali ambazo kibiashara zinatumia jina la Azam. Kampuni hizo zote zipo chini ya mwavuli mmoja ambao msingi wake ni uwekezaji katika sekta ya chakula na vinjwaji, vifungashio, Usafirishaji abiria majini, usafirishaji na majengo.
Baadhi ya kampuni hizo ni Azam Bevarages, Azam Marines, Azam Tv, Azam Football na SSB Flour, inayojihusisha na utayarishaji, usambazaji na uuzaji wa unga wa ngano na mahindi ndani na nje ya Tanzania.
Katika mahojiano maalumu na Blog hii, Meneja masoko wa SSB Flour, Omar Kuwe pamoja na mambo mengine anaeleza kuhusu utendaji, mikakati, ubora wa unga wa kampuni hiyo na changamoto wanazokumbana nazo sanjari na mchango wake katika kukuza uchumi wa taifa.
Anasema kuwa kuundwa kwa Azam Bakhresa Group Companies, kumetokana na ubunifu wa mwenyekiti mtendaji wa kampuni hizo, Saidi Salim Bakhresa anayemwelezea kuwa mjasiriamali anayependa kujifunza.
Kuwe anaeleza kuwa yeye ni mmoja wa watendaji wazalendo katika kampuni hizo akisimamia masoko ya unga wa ngano wa Azam akisema kuwa kazi yake kubwa ni kuhakikisha bidhaa hiyo inawafikia walaji ikiwa katika hali ya ubora wa hali ya juu. Anabainisha kuwa unga wa ngano na sembe za Azam ni bidhaa zinazozalishwa kwa kuzingatia na kufuata taratibu na kanuni za kiafya kimataifa.
“Tunazalisha bidhaa kwa kufuata viwango vilivyowekwa na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Shirika la Taifa la Viwango (TBS), pamoja na Shirika la Viwango la Kimataifa (ISO) kwa kuwa bidhaa hizo pia husafirishwa nje ya nchi. Mfano sembe yetu tunauza hata Uingereza ingawa siyo wakati wote,” anasema Kuwe.
Anafafanua kuwa asilimia 85 ya bidhaa inayozalisha kampuni yake ni unga wa ngano kutokana na mahitaji makubwa yaliyopo na asilimia iliyobaki (15) huzalisha Sembe.
“Tunazalisha unga wa ngano bora, hata sembe bora inayokubalika na kupata soko hata nje ya nchi, tumewekeza katika kuhakikisha Watanzania wanatumia unga halishi, pia tunalenga kuzalisha unga wenye virutubisho na thamani zaidi kwa mlaji, vilivyo salama bila kuwa na madhara kwa watumiaji,”anasema Kuwe akiongeza: “Watanzania na watumiaji unga wa ngano wetu wakumbuke, Azam ndiyo nyumbani.”
Anaweka wazi kwamba uwezo na aina ya mitambo inayotumika kuzalisha bidhaa hiyo ni vya hali ya juu vikiwa vya kisasa, vyenye ubora wa kimataifa.
Anabainisha kuwa kutokana na mahitaji makubwa na uzalishaji mdogo nchini, kampuni yake hulazimika pia kuagiza ngano kutoka nje ya nchi ili kukidhi haja ya soko, mbali na ile inayonunuliwa hapa nchini katika baadhi ya mikoa ikiwamo Arusha na Manyara.

Anataja baadhi ya nchi ambazo SSB Flour huagiza ngano kuwa ni pamoja na Canada, Australia, Urusi na Afghanistan akibainisha hatua mbalimbali inazopitia kabla ya kusagwa unga.
“Ngano ikishafika bandarini na kupakuliwa hupitia hatua mbalimbali, hatua hizo hufanyika pia kwa mahindi. Yote huchekechwa kutoa uchafu, kisha sumaku kubwa hutumika kubaini na kutoa vitu kama sindano au waya kabla ya kusafishwa na kupepetwa tena,” anasema Kuwe na kuongeza:
“Ikiwa safi, husagwa na kutengenezwa kulingana na mahitaji na ubora, hata muda wa matumizi pia hutegemea ubora na aina ya unga. Mfano unga wa sembe huweza kudumu na ubora wake hadi miezi sita tangu ilipotengenezwa, dona hukaa hadi miezi mitatu.”
Meneja masoko huyo anaeleza kuwa Azam pia inazalisha ngano yake katika nchi za Malawi, Msumbiji, Uganda na Rwanda kupitia viwanda vyake vilivyojengwa katika nchi hizo za Afrika.
Akizungumzia mchango wa kampuni yake kwa pato la taifa Kuwe anasema: “Mchango wetu ni mkubwa kwa pato la taifa bila shaka wanapotajwa walipa kodi wakubwa kampuni yetu Azama haikosi, hilo linadhihirisha tunavyochangia pato la taifa.”
Anaongeza: “Lakini pia tunatoa ajira katika taaluma mbalimbali hasa kwa vijana hivyo kuchangia taifa kupunguza tatizo la ajira na kupitia hao pia pato la taifa linaongezeka kwani nao ni walipa kodi. Kwa wastani wafanyakazi wote wa Azam wanafikia 6,000.”
Kuhusu changamoto Kuwe anasema kwamba katika biashara ni lazima kuwepo changamoto kwani bila hivyo biashara inaweza kuanguka. Anataja changamoto wanazokumbana nazo ni upande wa masoko na mazingira ya biashara akisema tatizo analoliona ni kutokuwepo kwa sera halisi hasa ya uzalishaji wa unga wa mahindi.
“Hata hivyo tunafanya kazi karibu na Serikali,” alisema Kuwe akifafanua kwamba pamoja na changamoto hizo kampuni hiyo imeweza kufikisha bidhaa zake na huduma maeneo mbalimbali ya nchi hata vijijini, huku unga wake wa ngano, mahindi na bidhaa nyingine zikikubalika kutokana na ubora wake.
Kwa mujibu wa maelezo binafsi ya kampuni hiyo, Bakhresa Group ni moja ya kampuni zinazoongoza Tanzania na Afrika Mashariki, ikiwa na historia ya kipekee kwa mmiliki wake kuanzia na biashara ya mgahawa mdogo Jijini Dar es Salaam katika miaka ya sabini, ambapo iliendelea kukua na kuongezeka hata kupata umaarufu kama familia ya kibiashara katika ukanda huo.
Shughuli za kampuni hiyo kwa sasa zimeenea nchini Tanzania, Uganda, Kenya, Rwanda, Burundi hata Zambia. Pia inafanya shughuli zake katika nchi za Malawi na Msumbiji huku ikiwa na malengo ya kupanua zaidi wigo wa biashara zake katika nchi nyingine.
Maelezo hayo yanaonyesha kuwa kiuchumi Azam Bakhresa Group inajivunia mapato yanayofikia Dola 600 milioni za Marekani kila mwaka, ambazo ni sawa na takriban Sh960 bilioni, huku pia ikijivunia kutoa ajira kwa watu wa kada mbalimbali wanaofikia 500,000.
Katika salamu zake kwa mwaka uliopita wa 2013, Mwenyekiti wa Azam Group Companies, Said Salim Bakhresa aliuelezea mwaka 2012 kuwa mwaka wenye Baraka kwa kampuni yake hata kuibuka na kuwa mmoja wa washindi wa tuzo za ubunifu wa kibiashara maarufu ya ‘G20 Challenge on Inclusive Business Innovation,’ iliyotangazwa na wanachama wa kundi hilo Juni mwaka 2012.

Alisema kuwa katika mwaka 2012, kampuni hiyo iliweka rekodi mpya ya kusambaza tani 750 za ngano kwa siku jijini Dar es Salaam, na tani 250 kwa siku za unga huo katika mji wa Nacala,nchini Msumbiji.
Bakhresa alisema kuwa wana mpango wa kuanzisha miradi katika nchi ya Burundi pia kupanua shughuli zake zaidi nje ya Ukanda wa Afrika Mashariki.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop