Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Serikali Mtandao (eGA) Dkt. Jabir Kuwe Bakari akitoa mada kuhusu matumizi ya “Broadband” katika shughuli za Serikali wakati wa mkutanao wa wadau wa Tehama nchini katika ukumbi wa NSSF Waterfront leo jijini Dar es salaam.
Kaimu
Katibu Mkuu Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Mh. John
Mngodo akiogea na wadau wa Tehama wakati wa ufunguzi wa mkutano wa wadau
hao leo jijini Dar es salaam.
Mkuu
wa kitengo cha cha ICT Broadband cha Taifa-TTCL Adin Mgendi akitoa
mada juu ya Wakati ujao tunaotaka kuuona wakati wa mkutanao wa wadau wa
Tehama nchini leo katika ukumbi wa NSSF Waterfront jijini Dar es salaam
na kubainisha kuwa TTCL imepanua wigo wa kutoa huduma ya mtandao wa
mawsiliano(internet) ndani na nje ya nchi, katika nchi jirani
zinazonufaika na huduma hiyo ni Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda, Malawi
na Zambia.
Kaimu
Mkurugenzi wa ICT Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Dkt.
Ally Simba (kulia) akifafanua jambo kwa washiriki wa mkutanao wa wadau
wa Tehama nchini katika ukumbi wa NSSF Waterfront leo jijini Dar es
salaam. Katikati ni Mkurugenzi wa Smile Communication Tanzania Ltd Mark
Redman, na wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Operesheni Mfuko wa Huduma za
Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) Albert Richard.
Baadhi
ya wadau wa Tehama nchini wakifuatilia na kumsikiliza Mgeni rasmi
Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Mh. John
Mngodo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa wadau hao leo jijini Dar es
salaam.
Kaimu
Katibu Mkuu Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Mh. John
Mngodo akiongea na waandishi wa habari mara baada ya ufunguzi wa mkutano
na wadau wa Tehama nchini leo jijini Da es salaam.(Picha zote na
Eleuteri Mangi – MAELEZO)
0 comments:
Post a Comment