Welcome to our online store Portal

Template Information

Wednesday, March 5, 2014

USAWA WA JINSIA NI WINGU ZITO BUNGE LA KATIBA

bunge
Bunge la Katiba linaloendelea mjini Dodoma.

Suala la Jinsia katika uongozi wa Bunge Maalum la Katiba limeibua Mjadala mzito katika nafasi ya Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa bunge hilo.
Mjumbe wa Bunge hilo Lediana Mung’ong’o ndiye aliyekuwa wa kwanza kuibua suala hilo wakati wa mjadala kuhusu marekebisho ya kanuni za bunge kipengele 8(i) kinachozungumzia utaratibu wa kumchagua Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti.
Mung’ong’o alitaka kipengele hicho kuzingatia uhusiano wa kijinsia, ambapo kama mwenyekiti atakuwa ni mwanaume, makamu wake awe mwanamke au kama Mwenyekiti atakuwa mwanamke, makamu wake awe mwanaume.

“Mwenyekiti hili suala la Mwenyekiti na Makamu wake hatuna budi kuangalia suala la jinsia kwamba ikiwa mwenyekiti atakuwa ni mwanaume, makamu wake awe mwanamke au kama Mwenyekiti atakuwa mwanamke, makamu wake awe mwanaume” amesema Mung’ong’o.
Naye Mjumbe wa Bunge hilo Anna Abdalah amesema kuwa suala hilo lilikosewa Tangu awali hivyo hakuna budi makubaliano yafanyike kwa busara maana wanawake wenye sifa na uwezo wapo wengi Tanzania Bara na Zanzibar.

Akichangia katika suala hilo Mjumbe wa Bunge Hilo ambaye ni Naibu Waziri Wizara ya Fedha Adam Malima amesema kuwa ili kuwepo kwa amani na Mshikamano sheria haina budi kusema wazi endapo Mwenyekiti atatoka Tanzania Bara basi Makamu wake atoke Zanzibar.
Akijibu hoja hiyo Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Othman Masoud Othman amesema kuwa suala hilo liwe la marekebisho lakini si kwa kuvunja sheria hiyo.
“Sharti hilo likibadilishwa litakuwa ni kituko na tutakuwa tunarekebisha sheria ambazo hazikutungwa na Bunge Maalum la Katiba hivyo ni busara kufanya makubaliano ili kufikia muafaka wa jambo hilo” amesemaOthman Masoud Othman.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop