Welcome to our online store Portal

Template Information

Monday, April 7, 2014

WANANCHI WA RWANDA WAKUMBUKA MAUAJI YA KIMBARI

http://azizicompdoc.blogspot.com/
Rwanda imekuwa ikilaumu Ufaransa kwa kilichotokea nchini humo
Rwanda inaadhimisha miaka 20 tangu kutokea mauaji ya kimbari mwaka 1994.
Watu laki nane waliuawa wengi wakiwa wa kabila la Tutsi na Wahutu wenye msimamo wa kadri. Wote waliuawa na watutsi wenye msimamo mkali.
Hii leo Rais Paul Kagame anatarajiwa kuwasha mwenge ambao utasalia hivyo kwa siku 100 , kipindi ambacho mauaji ya kimbare yalifanyika.
Mgogoro wa kidiplomasia umesababisha Waziri wa sheria wa Ufaransa, kujiondoa katika shughuli za kumbukumbu ingawa Ufaransa inasema kuwa balozi wake ataiwakilisha nchi hiyo.
Wengi wa waathiriwa wa mauaji ya Rwanda, walishambuliwa kwa mapanga kwa siku 100. Mauaji hayo yalianza Aprili mwaka 1994, punde baada ya kufariki kwa hayati Rais Juvenal Habyarimana.
  • 6 Aprili: 1994: Rais Habyarimana afariki katika ajali ya ndege
  • 7 Aprili: Wanajeshi wa Rwanda pamoja na waasi wawaua wananchi
  • 8 Aprili:Kundi la waasi la (RPF) laanza kupambana
  • 11 Aprili: Maelfu wauawa
  • 17 Mei: Baraza la usalama la umoja wa mataifa lasema mauaji ya kimbari yametokea
  • 22 Mei: RPF yadhibiti uwanja wa ndege wa Rwanda
  • 22 Juni: Mauaji ya watutsi yaendelea licha ya kuwepo wanajeshi wa Ufaransa nchini humo
  • 4 Julai: RPF yadhibiti Kigali
Alifariki wakati ndege yake iliposhambuliwa katika anga ya Kigali na kudunguliwa.
Baadhi ya viongozi wa kidini walihusishwa na ghasia zilizofuata kifo cha Habyarmana.
Mauaji ya kimbari yaliisha mwezi Julai 1994 wakati chama cha RPF, kilichokuwa cha waasi wa Tutsi wakati huo, kilipoingia nchini humo kutoka Uganda na kuchukua uongozi wa nchi hiyo.
Kumbukumbu zinaanza kwa kuwekwa mauwa katika eneo la kumbukumbu ya mauaji hayo na kufuatiwa na kuwashwa kwa mwenge katika uwanja wa michezo wa Amahoro mjini Kigali.
Mwenge huo umekuwa ukitembezwa katika nchi hiyo kwa miezi mitatu iliyopita
Viongozi wa kimataifa akiwemo waziri mkuu wa zamani wa Uingereza Tony Blair,aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini Thabo Mbeki na katibu mkuu wa UN Ban Ki-moon wanatarajiwa kuhudhuria hafla hiyo.
Mnamo Jumapili mamia ya watu walihudhuria maombi kuwakumbuka maelfu waliouawa

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop