Welcome to our online store Portal

Template Information

Saturday, June 21, 2014

SAMSUNG, BIDHAA MAALUM KWA MAZINGIRA YA AFRIKA


Print
Ukuaji endelevu wa uchumi wa Tanzania umeona ongezeko la kampuni za nje zikiingia nchini zikiwa na nia ya kuzindua bidhaa au huduma zao kwa Watanzania walio wengi. Mafanikio kwa bidhaa na huduma hizi yanategemea mambo mengi kuanzia mazingira hadi uhitaji, kuonyesha kwamba zinakubalika katika soko.

Kampuni moja ambayo imeona mafanikio yaliotulia na kua mtoa huduma tegemezi kwa Watanzania, ni kampuni ya vifaa vya umeme ya Samsung. Kupitia bidhaa zao mbalimbali wameshuhudia mauzo ya zaidi ya bidhaa zao 50,000 ndani ya mwaka mmoja. Katika mwaka ambao unatarajiwa kua wa mafanikio kwa kampuni hii Wanatazamia kudaka asilimia 30 ya soko la vifaa vya kielektroniki.
Takwimu hii inaweza kuja kama mshangao lakini ikiwekwa kwenye mtazamo halisi inajenga picha yenye uwazi. Mafanikio haya yanatokana na utafiti katika soko la Tanzania na bara la Afrika kwa ujumla.  Ukichanganya mambo kama vile uhitaji wa vifaa vinavyo okoa gharama na zenye uwezo wa kuhimili mazingira ya Kiafrika. Kampuni ya Samsung imeendelea kua mbele kutokana na ubunifu wa bidhaa ambazo kwa pamoja zajulikana kama “Built for Africa”. Sehemu ya friji ndio inazidi kupendwa na wateja wengi katika miaka michache iliopita kutokana na kuaminika na uwezo wa kuhimili mazingira ya Kiafrika. Katika kujengea mafanikio hayo, Samsung inaangalia kulenga soko kupitia aina mpya za friza zinazofaa kwa matumizi ya nyumbani na biashara. Uhitaji wa kuwa tofauti na asili ya uongozi ndio inaweka jina sokoni mpaka sasa.

Mkurugenzi Mtendaji wa Samsung Electronics Tanzania Bw. Dongha Jang aliunga mkono kauli zilizotajwa alipohojiwa na kusema “Samsung daima inatafuta kuunganisha wateja wake na bidhaa zake kwa kutoa bidhaa zinazosaidia kustawisha maisha ya mtumiaji. Sisi lengo letu ni kuleta teknolojia ya kisasa katika mfumo ambao ni muhimu zaidi kwa soko la Tanzania.” Mr. Jang alifafanua zaidi kuhusu uzinduzi wa bidhaa kadha moja kwa moja kwenye soko la Tanzania “katika hiki kipindi cha miaka michache iliopita tumeona umuhimu wa kuleta bidhaa mpya moja kwa moja kwa watumiaji wetu wa Tanzania kuliko kutegemea uzinduzi kwenye soko la kimataifa”. Miongoni mwa bidhaa Bw. Jang alizokuwa anaongelea katika msemo wake ni uzinduzi sambamba wa bidhaa mbili muhimu za nyumbani ambazo ni Samsung Duracool freezer na Triangle AC.

Uzinduzi huo ulikuwa sehemu ya mkakati wa kudumisha nafasi ya Samsung kama kiongozi wa vifaa vya umeme katika majumba ya Watanzania. Samsung Duracool freezer na Triangle AC zina sifa zinazoruhusu ufanyaji kazi kwa kiwango cha juu ukizingatia mazingira magumu ya Tanzania ikiwemo usambazaji wa umeme usioaminika na gharama zinazo panda. Samsung wanakuja na ahadi ya kurahisisha maisha kwa kuwa na bidha zenye gharama nafuu kwa mtumiaji.
Katika soko ambalo halitabiriki kama la Tanzania, kampuni hii ya vifaa vya umeme imeweza kutambua maeneo yaliokuwa ya maslahi kwa wateja wake kimahesabu. Hii ni dhahiri leo kupitia uwepo wake katika mitaa mbalimbali nchini. Katika mazingira ambayo hayana uhakika wa mafanikio kwa wote, Samsung inaendelea kushinikiza mipaka ya ubunifuu wa bidhaa  ambazo “zimetengenezwa kwa ajili ya Africa”.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop