Welcome to our online store Portal

Template Information

Tuesday, June 24, 2014

SUMATRA YAKAMATA MABASI 25 YA UDA JIJINI DAR

http://azizicompdoc.blogspot.com/
Mabasi mengine 25 ya Shirika la Usafiri Dar es Salaam (Uda), yamekamatwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri Majini na Baharini (Sumatra), kutokana na kuendelea kukaidi amri ya kuwataka wafuate sheria za usafirishaji wa abiria jijini.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Ofisa Mfawidhi wa Sumatra, Conrad Shio alisema mpaka sasa wameshayakamata mabasi 40, kati ya hayo, 15 yalikamatwa wiki iliyopita.
Madereva wa mabasi hayo wanadaiwa kufanya makosa tofauti ikiwa ni pamoja na kutokuwa na leseni ya uchukuzi wa abiria jijini Dar es Salaam, inayotolewa na mamlaka hiyo, stika na vibao vya kuonyesha njia wanazokwenda.
Shio alisema walipoyakamata awali na kuyaachia, uongozi uliahidi kutekeleza maagizo waliyopewa na Sumatra lakini hawajayatekeleza mpaka sasa.
Alisema pia wamesitisha kwa muda kazi ya kuyakamata na sasa wanaendelea na mazungumzo chini ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.
Alisema baada ya mazungumzo hayo, atakuwa katika nafasi nzuri ya kuweza kuzungumzia hatua zaidi ambazo watachukua au kile ambacho watakuwa wameafikiana kwa vyombo vya habari.
“Tumeona tusitishe operesheni hii ya kuyakamata mabasi haya ili kutoa nafasi ya mazungumzo chini ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa na iwapo mwafaka usipofikiwa tutajua cha kufanya” alisema Shio.
Kulingana na makosa ambayo yamekutwa katika mabasi hayo, kila basi litalazimika kulipiwa Sh250,000 na kwa mabasi 40, Uda watalazimika kulipia Sh10 milioni. Wiki iliyopita, Sumatra ilianzisha operesheni ya kuyakamata mabasi ya Uda kutokana na  malalamiko ya wananchi kuwa yamekuwa yakivunja sheria na hayana stika wala vibao vinavyoonyesha njia wanazopita.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop