Welcome to our online store Portal

Template Information

Wednesday, June 25, 2014

SISTA WA KANISA KATOLIKI APIGWA RISASI

http://azizicompdoc.blogspot.com/
Wananchi wakiangalia sehemu ambayo majambazi walimpiga risasi Sista Clencensia Kapuli Ubungo, Riverside, Dar es Salaam jana. Picha na Michael Matemanga 

Majambazi wamemuua kwa risasi Sista wa Kanisa Katoliki Clencensia Kapuli (50) na kupora kiasi kikubwa cha fedha ambacho hakijajulikana.
Pia, katika tukio hilo lililotokea jana saa nane mchana eneo la Riverside, Ubungo, Dar es Salaam, dereva aliyekuwa akimwendesha Sista Kapuli, Patrick Mwarabu alikatwa kidole gumba kwa risasi.
Sista Kapuli wa Shirika la Mtakatifu Maria wa Parokia ya Mwenyeheri Anwarite, Makoka Jijini Dar es Salaam alikuwa mhasibu wa parokia hiyo ambayo inamiliki Shule ya Sekondari Mwenyeheri Anwarite na Chuo cha Ufundi Stadi Makoka.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura aliyefika katika Kituo cha Polisi Urafiki kufuatilia tukio hilo alisema Sista Kapuli na sista mwenzake wakiwa katika gari aina ya Toyota Hilux, walikuwa wakitoka Benki ya CRDB, Tawi la Mlimani City kuchukua fedha na walipita Riverside ndipo walipopatwa na mkasa huo.
“Bado hatujajua ni kiasi gani cha fedha kimechukuliwa kwa kuwa Sista Kapuli ndiye alikuwa mhasibu na ndiye aliyekwenda kuchukua fedha hizo, subirini tutakapokwenda benki kuuliza ni kiasi gani cha fedha alichukua na tutawajuza,” alisema Wambura.
Kamanda huyo alisema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ukisubiri taratibu za mazishi.
Shuhuda wa tukio hilo, Gadi Kinyamagolo alisema masista hao walikwenda Riverside kununua mchele katika moja ya maduka ya jumla.
“Mara baada ya kumaliza kununua mchele kama kilo 10 hivi walipanda katika gari wakiwa wawili na kabla ya kuondoka zilifika pikipiki mbili zikiwa na watu wanne, zikasimamisha gari hilo huku mmoja akiwa amevalia kininja na mwingine aliyevaa kawaida, wote wakiwa na silaha. Wengine wawili walibaki kwenye pikipiki.
“Kisha nikaona wanapasua kioo cha nyuma ambapo kulikuwa na sista mmoja na mwingine alikuwa mbele, wote wakiwa na mikoba ambayo majambazi hao waliiomba,” alisema Kinyamagoro na kuongeza:
“Walianza kuwaambia tupe mikoba huku majambazi hao mmoja akiwa amesimama upande wa dereva na mwingine upande wa pili wa gari alipokuwa sista aliyeuawa lakini masista wale hawakutoa mikoba hiyo.”
Kinyamagoro alisema: “Baada ya mabishano, sista aliyekuwa nyuma alifungua mlango na kukimbilia katika duka walilonunua mchele na yule aliyekuwa mbele alipofungua mlango akitaka kukimbia alipigwa risasi shingoni na kutokea upande wa pili na kuanguka nje ya gari.
“Baada ya tukio hilo majambazi hayo yalichukua mikoba miwili na kuondoka nayo. Kwa kuwa mimi nilikuwa karibu nililala chini na eneo hili lilikuwa kimya, watu walikimbia na wengine tulilala tukaacha wafanye kazi yao.”

Shahidi mwingine, Saidi Juma alisema: “Wakati majambazi hao wakiondoka palikuwa na watu wawili waliovalia sare za Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) wakipita eneo hilo, waliulizwa na majambazi wanafanya nini huku wakiwa wameonyeshwa bunduki. Walinyoosha mikono juu na kuachwa, kisha majambazi wakapanda pikipiki zao na kutokomea.
“Wakati majambazi wakiondoka watu hao waliruka na kulala mtaroni kukwepa kupigwa risasi. Majambazi walipofika hapo mbele (mbele kidogo ya eneo la tukio), walimpiga risasi muuza machungwa na kumjeruhi begani.”

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop