Welcome to our online store Portal

Template Information

Tuesday, June 24, 2014

POLISI WATANGAZA HALI YA HATARI KUHUSU NGOMA YA KIGODORO

http://azizicompdoc.blogspot.com/
Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, Advera Senso akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam, jana. Picha na Venance Nestory 

Jeshi la Polisi nchini limetangaza kuanzishwa kwa operesheni maalumu ya kuwasaka wasanii wa ngoma wanaocheza wakiwa uchi maarufu kama kigodoro na kuwafikisha katika vyombo vya sheria.
Pia, litafanya operesheni ya kuwasaka madereva wa bodaboda, bajaji na baiskeli za matairi matatu wasiofuata sheria za usalama barabarani.
Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, Advera Senso alisema “Tunalaani vikali vikundi vya ngoma ambavyo hivi karibuni vimeibuka kwa wingi na huwa vinafunga mitaa na barabara huku wanawake wakicheza wakiwa uchi.’’
Hivi karibuni Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alipiga marufuku ngoma za aina hiyo.
Alisema kuwepo kwa vikundi hivyo ni uvunjaji wa sheria na maadili ya nchi, jeshi hilo litawasaka popote walipo ili kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria.
Alisema vikundi vya ngoma vinatakiwa kufuata utaratibu unaowekwa na halmashauri za maeneo husika ili kuzuia mianya ya kukiuka maadili.
Akizungumzia tukio la juzi la wachezaji wa kigodoro kudai kupigwa risasi eneo la Mwananyamala, alisema hakuna msanii aliyepigwa risasi, waliumia wakati wa purukushani zilizotokea polisi walipokuwa wakiwatawanya watazamaji wa ngoma hiyo.
“Hata ripoti ya daktari kutoka Hospitali ya Mwananyamala inaonyesha wacheza ngoma hao hawakupigwa risasi kama wanavyodai wao,” alisema Senso.
Akizungumzia operesheni ya bodaboda alisema, “Imekuwa  kawaida kwa madereva wa vyombo hivyo kupita barabarani wakati taa nyekundu zikiwa zinawaka hali ambayo husababisha ajali nyingi. kutokea.”
Alisema kuanzia Januari mpaka Juni, mwaka huu, ajali 1,449 zilizosababishwa na vyombo hivyo zilitokea na kusababisha vifo 218 huku watu 1,304 wakijeruhiwa.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop