Welcome to our online store Portal

Template Information

New Products
Showing posts with label Rage. Show all posts
Showing posts with label Rage. Show all posts

Saturday, December 28, 2013

RAGE APASUA JIPU

http://www.azizicompdoc.blogspot.com/
Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage amesema amesikitishwa na madai kuwa hakuhusika na ushindi dhidi ya Yanga.
Madai hayo yalitolewa na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo, Sued Nkwabi kwamba hakuhusika kufanikisha ushindi dhidi ya wapinzani wao, Yanga katika mchezo wa Nani Mtani Jembe ambapo Simba ilishinda 3-1.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Rage alisema anashangaa madai ya namna hiyo yanaelekezwa kwake Simba inapofanya vibaya licha ya kwamba yeye si kocha, lakini inapofanya vizuri huambiwa hahusiki.
“Nimewasikia hao wanaosema kwamba mimi sikuhusika na ushindi ilioupata Simba katika pambano dhidi ya Yanga. Huku ni kupotosha.
“Unawezaje kusema mimi sijahusika wakati hata mchezaji aliyefunga bao la tatu Awadh Juma nilimsajili mimi nyumbani kwangu? Na siyo bao la tatu tu, hata pasi ya bao la kwanza alilofunga Hamis Tambwe alitoa yeye,” alisema Rage na kuongeza:
“Kila mtu ana uhuru wa kuongea lakini tuwe wa kweli basi, ukisema Kamati ya Utendaji ya Simba ndiyo imefanikisha ushindi maana yake na mimi ni sehemu hiyo kamati inaonekana watu wengine hawaijui hata katiba ya Simba.”
Siku chache baada ya pambano hilo ambalo Simba iliibuka na ushindi wa mabao 3-1, Nkwabi alisema Rage hakuchangia kwa namna yoyote kufanikisha timu yao kuibuka na ushindi.
Rage yuko kwenye mgogoro na Kamati ya Utendaji ya klabu ya Simba baada ya wajumbe hao kumsimamisha uongozi wakati akiwa yeye hayupo kikaoni.
View detail

Wednesday, November 20, 2013

KILICHOMSIMAMISHA RAGE HIKI HAPA

Jana uongozi wa klabu ya Simba ulitangaza kumsimamisha mwenyekiti wake Ismail Aden Rage.
Maamuzi hayo yalitokana na kikao cha kamati ya utendaji kilichofanyika hapo juzi,
Hizi ni Miongoni mwa sababu zilizotolewa kwenye mkutano wa waandishi wa habari zilizopelekea kusimamishwa kwa Mheshimiwa Rage.
Mkataba na AZAM  TV
Rage alisaini mkataba na Azam TV kwa ajili ya kipindi ya cha Simba TV bila kuishirikisha kamati ya utendaji.
Wakati Rage anasaini mkataba na Azam TV tayari klabu ya Simba ilikuwa kwenye mazungumzo ya mwisho mwisho kuingia mkataba na kampuni ya ZUKU kwa ajili kipindi cha Simba TV uliokuwa na thamani ya dola za kimarekani 300,000 kwa mwaka.
Kampuni ya ZUKU ilipokuwa kwenye majadiliano na viongozi wa vilabu vya Simba na Yanga jijini Nairobi, kwenye mkutano huo Simba iliwakilishwa na Mjumbe wa kamati ya utendaji Joseph Itang’are maarufu kama mzee Kinesi pamoja na mwanachama Evans Aveva wakati Yanga iliwakilishwa na Makamu mwenyekiti Clement Sanga na Francis Kifukwe,viongozi hao Simba Ghafla walisikia Rage kasaini mkataba na Azam TV kwa ajili ya Simba TV.
Sakata la uhamisho wa Emmaanuel Okwi.
Mheshimiwa Rage ndiye aliyesimamia uhamisho wa mchezaji Okwi on CREDIT bila kuishirikisha kamati ya utendaji,matokeo yake klabu hiyo mpaka leo imeshindwa kupata pesa ya uhamisho wa mchezaji huyo.
Kutoitisha vikao vya kamati ya utendaji.
Sababu nyingine iliyoelezwa ni kitendo chake cha kushindwa kuitisha vikao vya kamati ya utendaji, Kuendesha klabu na kufanya maamuzi binafsi bila ya kushirikisha kamati hiyo ya utendaji ambayo ilichaguliwa na wanachama
Strategic plan ( Mpango mkakati )
Hivi karibuni klabu ya Simba ilizindua mchakato wa kutengeneza mpango mkakati (Strategic Plan) lakini cha kushangaza mwenyekiti amekuwa hataki kuona mpango huo ukifanikiwa.
Mkutano mkuu wa katiba
Kushindwa kuitisha mkutano wa marekebisho ya katiba,kuchukua maamuzi binafsi ya kuhairisha mkutano maalumu wa katiba uliotakiwa kufanyika Novemba, mwaka huu.
View detail

Tuesday, November 19, 2013

RAGE ASIMAMISHWA UONGOZI SIMBA


www.azizicompdoc.blogspot.com
Taarifa zilizothibitishwa kutoka Katika klabu ya Simba ni kwamba kamati ya utendaji ya klabu hiyo imemsimamisha mwenyekiti wa klabu Ismail Aden Rage kuongoza timu hiyo.
Kuhusiana na sababu zilizopelekea Rage kusimamishwa na kamati ya utendaji na Rage amechukuliaje uamuzi wa kamati ya utendaji, endelea kutembelea Blog yetu. Taarifa zaidi zitakujia.
View detail

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop