Jengo kuukuu
la Ghorofa 5 ambalo lilikuwa halijamalizika ujenzi wake lililopo eneo
la Sinza Mori karibu kabisa na Masjid Qubah,limeporomoka jioni hii na
kusababisha kifo cha mtu mmoja ambaye alikuwa na wenzake wawili jirani
na jengo hilo,ambapo mmoja alivyoona hatari hiyo alikimbia na kuwaacha
wenzie wawili ambao walinasa ndani Kati ya walionasa mmoja amefanikiwa kutolewa huku akiwa ameumia vibaya na mwingine ndio huyo aliepoteza maisha.
Inasemekana
chanzo cha kuanguka kwa jengo hilo la Ghorofa ni hali yake ya kukaa kwa
muda mrefu bila kumalizika kwa ujenzi waka ambapo inadaiwa kuwa lina
umri wa zaidi ya miaka 10.
0 comments:
Post a Comment