Mkuu
wa Kitengo cha Uzalishaji na Masoko wa DTB, Sylvester
Bahati,(kushoto)akiwaelezea waandishi wa habari,jinsi ya kutoa fedha
kwenye mashine za kutolea fedha za DTB kupitia huduma ya Vodacom M PESA
ambapo sasa wateja wanaotumia huduma hiyo wanaweza kutoa pesa kupitia
mashine hizo popote walipo nchini,huduma hiyo imezinduliwa leo jijini
Dares Salaam pamoja nae ni Meneja mahusiano ya nje wa Vodacom
Tanzania,Bw.Salum Mwalim.
Meneja
mahusiano ya nje wa Vodacom Tanzania,Bw.Salum Mwalim,akitoa fedha kwa
mara ya kwanza baada ya kuzinduliwa kwa huduma ya kutoa fedha kupia
mashine za kutoa fedha za DTB kupitia huduma ya M PESA, ambapo sasa
wateja wanaotumia huduma hiyo wanaweza kutoa pesa kupitia mashine hizo
popote zilipo nchini anaeshuhudia ni Mkuu wa Kitengo cha Uzalishaji na
Masoko wa DTB, Sylvester Bahati.
Meneja
mahusiano ya nje wa Vodacom Tanzania,Bw.Salum Mwalim,pamoja na Mkuu wa
Kitengo cha Uzalishaji na Masoko wa DTB, Sylvester Bahati.wakifurahia
mara baada ya kutoa fedha kwa mara ya kwanza kupitia mashine za kutoa
fedha za DTB kwa huduma ya M PESA, ambapo sasa wateja wanaotumia huduma
hiyo wanaweza kutoa pesa kupitia mashine hizo popote zilipo nchini.
Ukuaji
wa teknolojia ya huduma maarufu ya kutuma, kupokea fedha pamoja na
kufanya malipo ya huduma mbalimbali kwa njia ya simu za mkononi ya
kampuni ya Vodacom ya M-pesa inazidi kupanuka na hivyo kuongeza kiwango
cha matumizi ya huduma hiyo kuzidi kuboresha maisha na kuyafanya kuwa
rahisi zaidi.
Katika
kufikia mafanikio hayo Benki ya Diamond Trust (DTB) leo imetangaza ubia
wa kibiashara na kampuni ya Vodacom Tanzania ubia ambao unawawezesha
wateja wa M-pesa kuwa na uwezo wa kutoa fedha kutoka katika akuanti za
M-pesa kwa kutumia mashine za kutolea fedha (ATM) za benki ya Diamond
Trust.
Wakitangaza
na kuzindua huduma hiyo jijini Dar es salaam Mkuu wa Kitengo za
Uzalishaji na Masoko wa DTB, Sylvester Bahati, amesema hayo ni
mafanikio mengine ya kibishara kwa benki hiyo ya DTB katika kupanua wigo
wa huduma na namna benki hiyo inavyoweza kuunganisha teknolojia ili
kuleta urahisi kwa watanzania.
"DTB
inayo Furaha kubwa kuwa sehemu ya mapinduzi ya kiteknolojia hapa nchini.
Hii ni huduma ya kwanza na ya aina yake ambayo hakuna shaka kwamba
inaashiria uwezo wa DTB katika kuleta ufumbuzi wa namna bora ya kutumia
teknolojia kurahisisha maisha."Amesema Bahati
"Tukishirikiana
na Vodacom tunawawezesha wateja wa M-pesa walio karibu na benki zetu na
hususan mtandao wa ATM kuwa na uhakika wa kutoa fedha kutoka akaunti
zao za M-pesa saa ishirini na nne katika siku zote saba za wiki."
Bahati
amesema jambo hilo litasaidia kwa kiasi kikubwa kurahisisha upatikanaji
wa huduma za kibenki sanjari na kuboresha hali ya maisha na uchumi kwa
watanzania wote mijini na vijijini.
Hata
hivyo hii ni frusa ya kipekee kwa wateja wa benki ya DTB ambao
wamejiandikisha kwa ajili ya huduma ya M-Pesa hawana haja tena ya
kutembelea matawi ya benki hiyo ili kuweza kuweka amana zao au kuhamisha
fedha kwa biashara, marafiki na familia zao. Pia uzinduzi wa huduma
hiyo utawezesha kujenga urahisi wa kuruhusu wasiotumia huduma ya benki
kupata huduma za kifedha karibu nao.
Azma
ya DTB ni kuzidi kuongeza kasi na maboresho ya utoaji wa huduma kwa
wateja wake na washirika wake wengine kwa kuhakikisha inaendelea kupanua
wigo wa huduma zake ikiwemo kuongeza ATMs, matawi na huduma nyinginezo
kwa lengo la kusogeza karibu huduma za kibenki nchi nzima.
Kwa
upande wake Afisa Mkuu wa M- Biashara wa Vodacom Jacques Voogt, amesema,
"Hii ni hatua nyingine ambayo tunaifikia leo. Kampuni ya Vodacom
inaendelea kupanua mtandao wake wa huduma ya M-Pesa."
Voogtz ameongeza kuwa ubia huo ni mwendelezo wa azma ya kampuni ya
Vodacom kutumia fursa za teknolojia ya M-pesa kuzidi kuleta amsiha ya
watu mikononi mwao kutumia simu za kiganjani.
"Wateja
wa Vodacom M-pesa wanayo sababu nyingine ya kujivunia kuwa sehemu ya
mtandao mpana wa huduma hii salama, rahisi na yenye kuaminika zaidi
nchini wakiunganishwa na makampuni na hata tasisi zaidi ya 200 kufanya
malipo ya huduma na manunuzi kwa urahisi na wepesi zaidi kupitia simu za
viganjani."Aliongeza Voogtz
0 comments:
Post a Comment