"Somalia imepiga hatua" ASEMA DEVID CAMERON
Waziri Mkuu David Cameron asema Somalia imepiga hatua
Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron
amesema kuwa Somalia "imepiga hatua kubwa" katika kumaliza fujo na
machafuko yaliodumu kwa zaidi ya miongo miwili.
Bwana Cameron ni mwenyeji wa mkutano wa kutafuta amani ya kudumu nchini Somalia.
Mkutano huo unalengo la kumsaidia Rais Hassan Sheikh Mohamud aweze kuijenga tena upya Somalia.
Somalia inahesabiwa kuwa miongoni mwa mataifa
yalioanguka na ambayo imekuwa ikihangaishwa na magaidi wa Al shabaab,
uharamia na ukame ulioitikisa mwaka kati ya 2010 hadi 2012.
Rais Mohamud wa Somalia amesema serikali yake
itafaulu kuidhibiti nchi nzima na kukabiliana na utovu wa usalama
ifikapo mwaka 2015.
Mkutano huo utajikita zaidi katika masuala ya
kujenga upya vikosi vya ulinzi na kukabiliana na ubakaji ambalo ni suala
linalooonekana kama mwiko.
Takriban watu saba waliuawa katika mlipuko wa
bomu kwenye gari uliotokea katika mji mkuu Mogadishu siku ya Jumapili.
Kundi la Al - Shabab ambalo lina mafungamano na Al - Qaeda linadai
kuhusika na shambulio hilo.
Bofya hapa kusoma zaidi
Related Product :
Why Shop on Bongo Online?
We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be
0 comments:
Post a Comment