Waziri wa mambo ya ndani ya nchi, Dkt.Emmanuel Nchimbi
Na Immaculate Makilika-MaelezoSERIKALI imesema kuwa itachukua hatua kali kwa mtu yeyote bila kujali hadhi nafasi yake katika jamii kufuatia kuwepo kwa watu wachache wasiyoitakia mema nchi yetu kutaka kupandikiza chuki za kidini miongoni mwa Watanzania na kuleta mapigano, mauaji nchini
Kauli hiyo imetolewa leo Bungeni na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi wakati akitoa kauli ya Serikali kuhusu mlipuko wa uliotokea katika kanisa la katoliki la Mtakatifu Joseph Parokia ya Olasiti Arusha mjini Mei 5, mwaka huu saa 4:30 asubuhi na kusababisha vifo vya watu wawili na kujeruhi 59, kati ya hao watatu ni mahututi.
0 comments:
Post a Comment