Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (kushoto) akimpa cheti
mwanafunzi Nuru Ally aliyefanya vizuri kuliko wanafunzi wote katika somo
la Development Studies katika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine
kilichopo mjini Morogoro. Mwanafunzi huyo pia alikabidhiwa zawadi ya
Shilingi 50,000. Kushoto ni Makamu Mkuu wa Chuo-Taaluma SUA, Profesa
Peter Gillah. (Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya
Nchi).
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi akizungumza na wahadhiri
wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine pamoja na wanafunzi waliofanya
vizuri karika msomo mbalimbali wanaotarajiwa kufanya mahafali yao leo
tarehe 29, Novemba 2013 katika chuo hicho. Waziri Nchimbi alitoa vyeti
na zawadi kwa wanafunzi waliofanya vizuri katika msomo mbalimbali chuoni
hapo. Kulia ni Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Gerald Monela.
Kushoto ni Mkuu wa Jeshi la Magereza (CGP) John Minja na Makamu Mkuu wa
Chuo-Taaluma, Profesa Peter Gillah. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya
Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (wapili kushoto aliyevaa
tai) wakiwa katika picha ya pamoja na wahadhiri wa Chuo Kikuu cha
Kilimo cha Sokoine pamoja na wanafunzi waliofanya vizuri karika msomo
mbalimbali wanaotarajiwa kufanya mahafali yao leo tarehe 29, Novemba
2013 katika chuo hicho. Waziri Nchimbi alitoa vyeti na zawadi kwa
wanafunzi waliofanya vizuri katika msomo mbalimbali chuoni hapo. Picha
na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
0 comments:
Post a Comment