Welcome to our online store Portal

Template Information

Monday, November 18, 2013

WABUNGE WA AFRIKA MASHARIKI WANENA

IMG_1973
Mwenyekiti wa Wabunge wa Afrika Mashariki toka Tanzania, Alhaji Adam Kimbisa akizungumza na waandishi wa habari juu ya hotuba ya Mhe Rais Jakaya Kikwete na msimamo wa Watanzania katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, Kushoto ni katibu wa Wabunge wao,  Bi Shy-Rose Bhanji.
IMG_1996
 Katibu wa Wabunge wa Afrika Mashariki toka Tanzania Mh. Shy-Rose Bhanji (kushoto) akizungumzia umuhimu wa Amani katika Jumuiya ya Afrika Mashariki na nchi za maziwa makuu, Kulia ni Mwenyekiti wa Wabunge hao Alhaji Adam Kimbisa.
IMG_2004
Katibu wa Wabunge wa Afrika Mashariki -Tanzania Mh. Shy-Rose Bhanji akionyesha kitabu cha Mkataba wa Uanzishwaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwenyekiti wake Alhaji Adam Kimbisa.


WABUNGE wa Afrika Mashariki toka Tanzania wamesema mkataba wa uanzishwaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ni lazima uwe wa wananchi kwa manufaa ya wananchi (People Centred Integration) na isiwe ya viongozi. MOblog inaripoti.
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Wabunge wa Afrika Mashariki toka Tanzania, Alhaji Adam Kimbisa amesema wananchi washirikishwe katika kila hatua na kila ngazi ili waweze kushiriki kikamilifu kwa ajili ya maslahi yao.

“Jambo la msingi ambalo hata mkataba wa uanzishwaji wa jumuiya imesema wazi kwamba Jumuiya lazima iwe ni ya wananchi kwa manufaa ya wananchi na isiwe ya viongozi wa Afrika Mashariki,” amesema Kimbisa.
Amesema Wabunge wanaoiwakilisha Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki wanampongeza Rais Jakaya Kikwete kufuatia hotuba yake aliyoitoa bungeni mjini Dodoma hivi karibuni na kuelezea masuala kadhaa ya utengamano baina ya nchi wanachama wa Afrika Mashariki.
Kimbisa alisisitiza kuwa Rais alifanya uchambuzi wa kina kuhusu matatizo yaliyoikumba jumuiya kufuatia mikutano mitatu iliyofanywa na nchi tatu za Kenya, Uganda na Rwanda ikiwatenga Tanzania na Burundi.

Amesema vile vile kuweka wazi msimamo sahihi wa Tanzania kuendelea kuwepo katika Jumuiya ya Afrika Mashariki na kwamba Tanzania haitajitoa.
Kwa Upande Katibu wa Wabunge wao wa Afrika Mashariki, Bi Shy-Rose Bhanji amesema kama wabunge wanampongeza Mhe Rais Kama Amiri Jeshi Mkuu wa Kupeleka kikosi kimoja cha wanajeshi katika Brigedi Maalum iliyoundwa na Umoja wa Mataifa ili kuongeza nguvu ya udhibiti wa waasi Mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
“sisi tunaamini amani ni jambo la msingi katika Afrika Mashariki na hasa katika nchi zilizo katika maziwa makuu, tunawapongeza wanajeshi wetu na wanajeshi maalum wa umoja wa mataifa kwa kazi nzuri walioifanya,” 

“Tunaamini kwamba suluhisho la matatizo ya nchi za maziwa makuu yatapata ufumbuzi wa kudumu iwapo kutakuwa na utaratibu wa kukaa meza moja kwa pande zote husika na kufanya mazungumzo ya kuleta Amani,” amesema Bhanji.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop