Welcome to our online store Portal

Template Information

Tuesday, November 19, 2013

WAZIRI MKUU AONGOZA MAZISHI YA DKT MVUNGI

Mvungi Mwanga 9

Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Arusha Josephat Lobullu (kulia) na Askofu wa Jimbo la Same Rogath Kimaryo wakiongoza ibada ya mazishi ya aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Dkt. Sengondo Mvungi. Ibada hiyo ilifanyika katika kijiji cha Chanjale wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro na kuhudhuriwa pia na Askofu Damian Dallu (katikati) wa Jimbo la Geita Jumatatu, Novemba 18, 2013.
Mvungi Mwanga 5
 Waziri Mkuu Mizengo Pinda, mkewe Mama Tunu, Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Joseph Warioba na viongozi wengine wakifuatilia ibada ya mazishi ya aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Dkt. Sengondo Mvungi. Mazishi hayo yalifanyika kijijini Chanjale wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro JUmatatu, Novemba 18, 2013.
Mvungi Mwanga 8
Familia ya aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Dkt. Sengondo Mvungi ikifuatilia ibada ya mazishi iliyofanyika katika kijijini cha  Chanjale wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro Jumatatu, Novemba 18, 2013.
Mvungi Mwanga 4
Jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Dkt. Sengondo Mvungi likishushwa kaburini wakati wa mazishi yaliyofanyika kijijini Chanjale wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro  JUmatatu, Novemba 18, 2013.
Mvungi Mwanga 1
Askofu Damian Dallu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Geita akiongoza ibada ya mazishi ya aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba marehemu Dkt. Sengondo Mvungi katika makaburi ya familia kijijini Chanjale wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro Jumatatu, Novemba 18, 2013.
Mvungi Mwanga 2
Mke wa aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba marehemu Dkt. Sengondo Mvungi, Bi. Anna Mvungi akiweka shada la maua katika kaburi la mume wake wakati wa mazishi kijijini Chanjale wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro Jumatatu, Novemba 18, 2013.
Mvungi Mwanga 3
Waziri wa Uchukuzi Dkt. Harrison Mwakyembe na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi James Mbatia wakiweka shada la maua katika kaburi la aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Dkt. Sengondo Mvungi wakati wa mazishi kijijini Chanjale wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro Jumatatu, Novemba 18, 2013.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda jana (Jumatatu, Novemba 18, 2013) aliongoza mamia ya waombolezaji katika mazishi ya aliyekuwa Mjumbe wa Tume na Mabadiliko ya Katiba na Kiongozi wa NCCR-Mageuzi Dkt. Sengomdo Mvungi yaliyofanyika katika kijiji cha Chanjale wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro.
Pamoja na Waziri Mkuu aliyeongozana na mkewe, Mama Tunu, pia walikuwepo Mawaziri kadhaa kiwemo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Uratibu na Uhusiano) Steven Wassira aliyekabidhi ubani wa Rasi Jakaya Kikwete kwa familia.

Ibada ya mazishi iliendeshwa na Maaskofu watatu wakiongozwa Askofu Mkuu wa Jimbo la Kanisa Katoliki Arusha, Josephat Lebullu ambaye ni mwenyeji wa wilaya ya Mwanga. Wengine walikuwa Askofu wa Jimbo la Same Rogath Kimaryo na Askofu wa Jimbo la Geita Damian Dallu aliyesafiri kutoka Geita kuja kuungana na wenzake kumuaga Dkt. Mvungi.
Pamoja na Waziri Mkuu, mazishi hayo pia yalihudhuriwa na zaidi ya nusu ya wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba wakiongozwa na Mwenyekiti wake Jaji Joseph Warioba. Mawaziri wengine waliokuwepo ni Prof. Jumanne Maghembe (Maji) ambaye pia ni Mbunge wa Mwanga.

Wengine ni Dkt. Harrison Mwakyembe (Uchukuzi) na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Angellah-Jasmine Kairuki. Pia walikuwepo Wakuu wa mikoa ya Arusha (Mugessa Mwalongo) na Kilimanjaro Leonidas Gama.
Kwa upande wa NCCR-Mageuzi, uongozi wote wa juu wa Chama hicho ulikuwepo ukiongozwa na Mwenyekiti wake James Mbatia ambaye aliiomba Serikali kuimarisha ulinzi na usalama wa wananchi na mali zao.

Pamoja nao, kulikuwa na wawakilishi kadhaa wa taasisi mbalimbali ambazo marehemu Dkt. Mvungi alifanya nazo kazi wakati wa uhai wake. Taasisi hizi ni pamoja na Chuo Kikuu cha Dar es salaam ambacho kiliwakilishwa na Mkuu wa Shule Kuu ya Sheria Prof. Bonaventure Rutinwa, Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kilichowakilishwa na Mkurugenzi Mtendaji Dkt. Hellen Kijo-Bisimba; Chuo Kikuu cha Bagamoyo (UB) na Chama cha Wanasheria Tanzania Bara (TLS) kilichowakilishwa na Wakili Eric Ngimaryo na mawakili wengine kadhaa kutoka mikoa ya Kilimanjaro na Arusha.

Dkt. Mvungi alifariki nchini Afrika Kusini alikokuwa amepelekwa kwa ajili ya uchunguzi na matibabu Zaidi akitokea Kitengo cha Mifupa Muhimbili (MOI) alikokuwa amelazwa baada ya kuvamiwa nyumbani kwake Kibamba, wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam na watu waliomjeruhi vibaya kichwani usiku wa kuamkia siku ya Jumapili, Novemba 3, 2013.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop