Azam
Media Ltd imepata leseni kutoka Mamlaka ya Mawasilino Tanzania (TCRA)
na hivyo kuwa na uwezo wa kuanza rasmi shughuli zake hapa Tanzania.
Hatua
hii muhimu sasa inaiwezesha AzamTV kuanza kutoa huduma zake kwa wateja
wake kote Tanzania kuanzia tarehe16 Desemba. Huduma hii itwapa fursa
wateja kuangalia zaidi ya chaneli 50 za kitaifa na kimataifa
ziliozosheheni burudani kwa ajili ya familia kwa bei nafuu ya shilingi
12,500/= kwa mwezi.
Kutakuwepo wigo mpana wa kuchagua kifaacho kuangalia
vikiwemo vipindi vya michezo, makala, watoto na tamthilia kutoka
Tanzania, barani Afrika na sehemu mbalimbali za dunia. Baadhi ya
vipindi hivyo tajwa vitapatikana katika chaneli maarufu kama vile
National Geographic Gold na Nickelodeon, na pia matangazo yetu yatakuwa
na chaneli za bila malipo zikiwemo TBC1, Channel 10, Clouds, ZBC na K24.
Jambo la kusisimu zaidi ni kwamba AzamTV itakuwa na matangazo katika chaneli zake tatu:
AzamOne
– Itakuwa na vipindi vya kiafrika, ambapo kwa asilimia kubwa vitahusu
masuala ya Afrika Mashariki kwa lugha ya Kiswahili. Hii ndiyo chaneli
ambayo itakuwa ikirusha matangazo ya Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara;
AzamTwo
– Hapa vitapatikana vipindi vya burudani kwa familia amabavyo ni vya
kimataifa na baadahi ya hiovyo vitakuwa katika lugha ya kiswahili;
SinemaZetu – Chaneli maalum kwa ajili ya tamthilia za kitanzania.
Mtendaji
Mkuu wa Azam Media, Rhys Torrington, alisema: “Huu ni wakati wa
kujivunia kwa Tanzania kwani sasa ina huduma za luninga zinazopatikana
kwa bei ambayo wengi wanaweza kuimudu. Miezi michache ijayo tutaivusha
huduma hii mipaka hadi katika nchi zingine za Afrika Mashariki na hata
mbali zaidi.
Nimefarijika kwamba tumewekeza vilivyo katika chombo hiki
cha kitanzania na tutaendelea kufanya hivyo”.
Torrington
pia alibainisha kuwa kwa wateja ambao hawatapenda kungojea kuzinduliwa
rasimi wa huduma za Azam TV, milango ya ofisi zake za Dar es Salaam
itakuwa wazi kuanzia (Ijumaa Desemba 6, 2013). Wateja wataweza
kununua vifaa muhimu kutoka duka la AzamTV na kwa mawakala
walioidhinishwa na hivyo kuweza kujionea vipindi mbalimbali kuanznia
sasa – japo malipo yao kwa mwezi yatahesabiwa kuanzia Desember 16.
0 comments:
Post a Comment