Mkurugenzi
wa chuo kikuu huria tawi la mkoa wa Singida, Bw. Mbaraka Msangi, akitoa
taarifa yake kwenye sherehe za kuwapongeza wahitimu 52 wa chuo hicho
zilizofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa kanisa Katoliki mjini
Singida.
Mkuu
wa mkoa wa Singida, Dk.Paresko Vicent Kone, akizungumza kwenye kilele
cha sherehe ya kuwapongeza wahitimu wa chuo kikuu huria cha mkoa wa
Singida,zilizofanyika mwishoni mwa juma mjini Singida.Wa kwanza kulia ni
mkurugenzi wa chuo hicho,Mbaraka Msangi.
Mkuu
wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone (kushoto) akimkabidhi Mwalimu Allan
Jumbe cheti cha kuhitimu chuo kikuu huria mjini Singida.Kwa mwaka
huu,jumla ya wanafunzi 52 wamefanikiwa kuhitimu katika chuo hicho.
Mkuu
wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone, (wa pili kulia) akiwa kwenye picha
ya pamoja na baadhi ya wahitimu wa chuo kikuu huria tawi la Singida.
Sherehe ya kupongeza wahitimu hao,ilifanyika kwenye ukumbi wa mikutano
wa kanisa katoliki mjini Singida.(Picha na Gasper Andrew).
Na Nathaniel Limu, Singida
Mkuu
wa Mkoa wa Singida,Dk.Parseko Vicenti Kone amewakumbusha wakazi wa mkoa
huo umuhimu wa kujiunga na chuo kikuu huria tawi la mkoani humo ili
kujiendeleza kielimu.
Amesema
kujiendeleza kielimu kutasaidia mhusika kujijengea mazingira mazuri ya
kumudu maisha yake kwenye dunia hii iliyojaa ushindani wa kila aina.
Dk.Kone
ametoa wito huo hivi karibuni wakati akizungumza kwenye hafla fupi ya
kuwapongeza wahitimu wa chuo kikuu huria kituo cha mkoa wa Singida wa
mwaka jana.
Amesema
changamoto zinazojitokeza hivi sasa Tanzania,Afrika mashariki na
duniani kwa ujumla pamoja na maendeleo ya kisayansi na teknolojia
zinatulazimisha sisi wote kuwa na elimu ya kutosha ili kuzikabili.
“Watanzania
tusipokuwa na elimu ya kutosha tutaachwa mbali sana na wenzetu wa nchi
zinazotuzunguka na wa dunia kwa ujumla.Tusisubiri jambo hili likatokea
ili hata jumuiya ya Afrika mashariki itakapokamilika tusije tukakuta
nafasi nyingi za kazi zinachukuliwa na wenzetu badala ya vijana
wetu,alifafanua Mkuu huyo wa mkoa.
Dk.Kone
amesema kutokana na ukweli huo wazazi na walezi wanalo jukumu la
kuwashauri na kuwahimiza vijana wao kujiendeleza kwa nguvu zote ili
kupata elimu inayokidhi mahitaji ya sasa na yajayo.
Katika
hatua nyingine, Mkuu huyo wa mkoa amewataka kupuuza dhana potofu kuwa
elimu inayotolewa na chuo kikuu huria siyo ya kiwango cha juu bali ni ya
kihuria huria tu.
“Dhana
hii potofu inayoenezwa kwa lengo la kuwakatisha tamaa Watanzania walio
wengi wasipate elimu ya juu ili kuwe na wachache tu waliosoma na walio
wengi wabakie bila elimu”,amesema.
Awali
Mkurugenzi wa kituo cha Chuo Kikuu Huria Mkoa wa Singida,Mbaraka Msangi
amesema wahitimu wa mwaka huu ni 56 wakilinganishwa na 46 wa mwaka
jana.Toka kituo hicho kianzishwe mwaka 2000,hadi sasa wahitimu
wameishafikia 263.
0 comments:
Post a Comment