Welcome to our online store Portal

Template Information

Monday, January 6, 2014

MJOMBA WA RAIS WA KOREA YA KASKAZINI ALIWA NA MBWA 120

http://azizicompdoc.blogspot.com/http://azizicompdoc.blogspot.com/
.walimvua nguo na kumtupa kwenye ngome ya Mbwa wenye njaa 120
.Rais Kim Jong Un alikataa mjomba wake kunyongwa bali kuliwa na mbwa akiwa uchi wa mnyama
.kiongozi huyo na viongozi wengine 300 walishuhudia ukatili huo wa kutisha
.Adhabu hiyo iitwayo ‘Quan jue’ ilidumu kwa saa moja
.Mjomba wake alishtakiwa kwa hila na rushwa na matumizi mabaya ya madaraka
Na Damas Makangale, kwa Msaada wa Mtandao
Taarifa zilizovuja kutoka mashirika mbalimbali ya habari duniani ni kwamba Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-Un alishuhudia jinsi mjomba wake Jang Thaek akiliwa na mbwa karibu 120 akiwa uchi wa mnyama kama adhabu mbadala badala ya kunyongwa.
Taarifa zinasema kuwa kiongozi huyo wa Korea Kaskazini aliamuru mjomba wake avuliwe nguo zote na kubaki uchi wa mnyama na kisha mbwa kumtafuna akiwa hai mpaka kifo chake, watetezi wa haki za binadamu wanasema ni adhabu ya kikatili ambayo dunia haijawahi kushuhudia kwa miongo kadhaa.
Watu wa karibu na wanafamilia wanasema Mjomba wake huyo alipelekwa kwenye ngome hiyo na wasaidizi wake watano na kuachiwa kwa mbwa wenye njaa ya siku tatu ili waweze kumshughulikia.
http://azizicompdoc.blogspot.com/

Mmoja wa Mbwa Mwitu aliyekaa na njaa kwa siku tatu ambaye alitekeleza hukumu ya Jang Song-Thaek mjomba wa Rais wa Korea ya Kaskazini.
Maelezo ya kutisha yaliojitokeza katika ripoti katika gazeti la Straits Times la Singapore , ambayo lilisema kitendo hicho ni cha  kutisha na kinajulikana kama ‘ Quan jue ‘, au ‘ utekelezaji wa adhabu kwa kutumia mbwa wenye njaa.
Thaek , alivaa suti ya bluu na pingu akisindikizwa katika mahakama ya Desemba 12, aliuawa na mbwa mwitu , kulingana na ripoti kutoka China.
http://azizicompdoc.blogspot.com/
Thaek , alivaa suti ya bluu na pingu akisindikizwa katika mahakama ya Desemba 12, aliuawa na mbwa mwitu , kulingana na ripoti kutoka China.
Taarifa zinaongeza kiongozi huyo wa Korea ya Kaskazini Kim Jong- Un alikuwa anatoa ujumbe katika sikukuu ya mwaka mpya kwa wakorea wote nchini humo.
Wachambuzi wanasema kiongozi huyo jeuri alikuwa na ujumbe maalum kwa viongozi walioalikwa kwenye sherehe ya kifo cha mjomba wake kama onyo kwamba wanapaswa kufuata taratibu na endapo kiongozi yeyote atakiuka taratibu adhabu kali itachukuliwa dhidi yake.
http://azizicompdoc.blogspot.com/
Kim Jong-Un akiwa na mjomba wake enzi za uhai wake.
http://azizicompdoc.blogspot.com/
Kim Jong-Un, akitoa hotuba kwa taifa hilo siku ya sikukuu ya mwaka mpya.
http://azizicompdoc.blogspot.com/
Baadhi ya viongozi wa ngazi za juu wa Korea ya Kaskazini ambao walishuhudia adhabu hiyo ya kikatili.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop