Welcome to our online store Portal

Template Information

Thursday, February 27, 2014

KIKWETE ANGURUMA WARAKA WA CCM

http://azizicompdoc.blogspot.com/

Waraka unaodaiwa kuandaliwa na CCM kwa ajili kuwaelekeza wajumbe wake kwenye Bunge Maalumu la Katiba kutetea msimamo wa Serikali mbili umepokewa kwa hisia tofauti huku Rais Jakaya Kikwete akitakiwa kujitokeza hadharani kueleza msimamo wake.
Waraka huo uliibuliwa na Blog hii jana ukibainisha sura ya Serikali mbili inayotakiwa na CCM, likiwamo pendekezo la kuanzisha Baraza la Wawakilishi la Tanzania Bara.
Miongoni mwa waliozungumzia waraka huo ni Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbrod Slaa ambaye amemtaka Rais Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM kutoka hadharani na kuweka wazi msimamo wake kuhusiana na mchakato wa Katiba Mpya.
Dk Slaa alieleza kushangazwa kwake na hatua ya CCM kuandika waraka aliodai umebadili vipengele vyote muhimu katika Rasimu ya Pili ya Katiba iliyoandaliwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba baada ya kukusanya maoni kwa wananchi.
Pia amemtaka Rais Kikwete kutozindua Bunge Maalumu la Katiba linaloendelea mjini Dodoma kwa madai kwamba kiutaratibu, linajitegemea na hata katika historia ya Katiba zilizowahi kuandikwa hazijawahi kusainiwa na rais.
Dk Slaa alitoa kauli hiyo jana wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wa kumnadi mgombea ubunge katika Jimbo la Kalenga, Iringa kupitia Chadema, Grace Tendega uliofanyika katika Kijiji cha Tanangozi, Kata ya Mseke.
Alisema Rais Kikwete na chama chake wanataka kubadili mambo yote muhimu yaliyoandikwa katika Rasimu ya Pili inayojadiliwa mjini Dodoma, huku akijua kuwa zaidi ya asilimia 60 ya Watanzania ndiyo waliotoa maoni.
Wengine wauponda
Mjumbe wa Bunge la Katiba, James Mbatia alisema ushawishi katika jambo lolote siyo dhambi, lakini hakutarajia ushawishi huo kufanywa na CCM, tena katika jambo nyeti kama mchakato wa Katiba.
“Kama suala ni Serikali tatu, hayakuwa mapendekezo ya Jaji Warioba, bali ya tume nyingi zilizowahi kuundwa na Serikali inayotokana na chama hicho tawala. Kuna Tume za Jaji Robert Kisanga, Francis Nyalali, William Shelukindo, Amina Salum Ali na sasa Joseph Warioba. Zote hizi zimependekeza Serikali tatu.”
Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Julius Mtatiro alisema CCM kutengeneza waraka huo ni sawa na `utekaji nyara’ wa maoni ya wananchi na kuweka maoni ya wana CCM katika Katiba Mpya.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Helen Kijo-Bisimba alisema kitendo cha CCM kutengeneza waraka wake ni kukwamisha upatikanaji wa Katiba bora.

“Hakukuwa na sababu ya kuweka Tume ya Mabadiliko ya Katiba iwapo nao wanakuja na waraka wao, tunatakiwa kuboresha yaliyomo kwenye rasimu ili tuweze kupata Katiba yenye maoni ya watu,” alisema.
Profesa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Gaudence Mpangala alisema iwapo CCM kimesambaza waraka huo, kinafanya makosa kwa kuendeleza misimamo isiyokuwa na hoja za msingi kwa Watanzania... “CCM kusambaza waraka huo ni dalili mbaya za kuleta machafuko miongoni mwa wajumbe...”
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), Nicholas Mgaya alisema hatua ya CCM kusambaza waraka huo ni kutapatapa kwa kuwa yaliyomo hayatawezekana kupitishwa na Watanzania.
Mgaya alisema waraka huo umevunja Sheria ya Mabadiliko ya Katiba inayozuia kusambaza maoni ya makundi katika mchakato huo.
Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba, Deus Kibamba alisema tatizo siyo kuwa na msimamo wa chama kupitia waraka huo, bali kuusambaza... “Sijaupata waraka huo lakini kitendo cha kuusambaza tu kisheria ni makosa, walitakiwa kutumia nafasi na wajumbe wake kupeleka hoja hizo bungeni,” alisema Kibamba.
Wabunge CCM wanena
Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai alisema katika hali ya kawaida, kila kundi katika jamii lina fikra zake kuhusu mapendekezo yaliyomo katika Rasimu ya Katiba na haki ya kupendekeza kile ambacho linaona kinafaa kuongezwa au kuondolewa na kwamba kuwa na mtazamo tofauti kuhusu jambo fulani ni kitu ambacho hakizuiliki.
“Binafsi ningependa kupata waraka kutoka kila kundi ili nisome na kujua mawazo mazuri yaliyopendekezwa. Ukipitia ni wazi kuwa utakutana na mambo mazuri tu. Hili ni jambo ambalo lipo wazi kabisa.”
Hata hivyo, Ndugai ambaye pia ni Mbunge wa Kongwa (CCM) alisema chama hicho hakijagawa rasimu yoyote.
Mbunge wa Nzega, Dk Hamisi Kigwangalla alisema hana hakika iwapo waraka huo umesambazwa kwa wajumbe.
Mbunge wa Nkasi Kaskazini, Ali Keissy naye alisema hajauona waraka huo, kauli ambayo iliungwa mkono na Mbunge wa Muleba Kaskazini, Charles Mwijage.
Jana, Blog hii ilichapisha taarifa za kuonekana kwa waraka huo, ambao pamoja na mambo mengine, umetoa mapendekezo katika ibara 42 za Rasimu ya Katiba ya Tume na kupangua hoja mbalimbali ikiwamo ya muundo wa muungano huku ikitaka mfumo wa Serikali mbili uendelee lakini ufanyiwe marekebisho.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop