Welcome to our online store Portal

Template Information

Thursday, February 27, 2014

MAGHOROFA MANNE DAR YATUMIA UMEME ZAIDI YA UTUMIWAO MTWARA

http://azizicompdoc.blogspot.com/

http://azizicompdoc.blogspot.com/

http://azizicompdoc.blogspot.com/
Ghorofa nne za kisasa zilizopo Dar es Salaam, zinatumia kiasi kikubwa cha umeme kuliko ule unaotumiwa katika Mkoa wa Mtwara.
Majengo manne ya PSPF Twin Tower, Uhuru Height, Viva Tower na Benjamin Mkapa Tower yote kwa pamoja yanatumia megawati 12 za umeme wakati mkoa huo unatumia megawati nane.
Kiasi hicho cha umeme kinachotumiwa na majengo hayo ni karibu sawa na umeme unaotumiwa na mkoa huo na Lindi kwa pamoja.
Aidha, majengo matatu ya PSPF Twin Tower, Uhuru Height na Viva Tower kwa pamoja yanatumia umeme mwingi kuliko ule unaotumiwa na baadhi ya mikoa nchini kama Ruvuma, Manyara, Singida, Kigoma na Rukwa.
Akizungumza katika mahojiano maalumu hivi karibuni, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania Tanesco, Felchesmi Mramba alisema PSPF peke yake linahitaji megawati tano na Uhuru Height megawati 2.5, Viva Tower megawati 2.5 na Benjamin Mkapa Tower megawati mbili.
Alitaja matumizi ya umeme katika mikoa hiyo na megawati zake kwenye mabano kuwa ni Manyara (10) Mtwara (8), Singida (7), Lindi (5.5), Kigoma (6), Ruvuma (4.7) na Rukwa (6.8).
Alisema Dar es Salaam inaongoza kwa kutumia umeme mwingi na kwamba mahitaji ya nishati hiyo yamekuwa yakiongezeka kutokana na ukuaji wa haraka wa sekta ya ujenzi.
Dar es Salaam pekee, kwa mujibu wa takwimu za Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) matumizi yake ni kati ya megawati 450 na 500 kwa siku, kiasi ambacho ni zaidi ya nusu ya umeme unaozalishwa na shirika hilo.
Alisema hivi sasa umeme unaozalishwa ni wastani wa megawati 1,100, huku sehemu kubwa ya nishati hiyo ikitokana na mitambo inayotumia gesi na mafuta.
Kutokana na hali hiyo, alisema Tanesco imeamua kutekeleza miradi 13 ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya umeme ikiwamo kuongeza uwezo wa njia za kusambaza na kukarabati. Pia kujenga vituo vipya vya kupozea umeme katika sehemu mbalimbali za Dar es Salaam.
“Baadhi ya majengo makubwa Dar es Salaam yanahitaji umeme mwingi. Unakuta jengo moja kama haya maghorofa linahitaji megawati nyingi za umeme kuliko zinazotumiwa na baadhi ya mikoa,” alisema Mramba na kuongeza:
“Ndiyo maana tunatekeleza miradi mingi ya kuongeza uwezo wa njia za kusambaza umeme maana mfumo tulionao sasa ni chakavu na hauwezi kuhimili kiasi cha umeme kinachotakiwa na watumiaji wa makundi mbalimbali.”

Mramba alisema uchakavu wa miundombinu na mahitaji makubwa ya umeme ni miongoni mwa sababu za umeme kukatika ovyo na kwamba njia za kuusafirisha hazina uwezo wa kuhimili kiasi kinachotakiwa.
Ili kukabiliana na hali hiyo, alisema shirika lake linatekeleza miradi inayojumuisha ukarabati wa vituo vya kusambaza umeme ambao utahusisha vituo vikubwa na vidogo katika maeneo ya Mwananyamala, Jangwani Beach, Kigogo, Tegeta, Muhimbili, Luguruni, Mikocheni, Kurasini, Mbagala, Gongo la Mboto na Kipawa.
Mramba alisema Kituo cha Gongo la Mboto kitahudumia wakazi wa Wilaya ya Kisarawe, Pwani, Segerea na Kinyerezi na katika Kituo cha Kipawa, Tanesco itaweka ‘saketi’ mbili kutoka Ubungo ili kutosheleza mahitaji ya viwandani na kusaidia kuwapo kwa umeme wakati wote endapo njia (line) moja itapata hitilafu.
“Njia (line) nyingine itaanzia kwenye Kituo cha Ilala, karibu na TBL kwenda katikati ya jiji mpaka Makumbusho na kurudi Ubungo. Mradi huu utakamilika Aprili, mwaka huu.

Pia utahusisha eneo la Mwenge, Tandale, Mikocheni, Masaki, Oysterbay ili wakazi wa maeneo hayo wapate umeme wa uhakika,” alisema.
Pamoja na vituo hivyo, Tanesco inajenga kituo cha kisasa eneo la Mikocheni, ambacho kitatumika kubaini maeneo yenye matatizo katika njia za usambazaji wa umeme... “Hivi sasa line (waya) ya umeme ikikatika, hatuwezi kujua tatizo liko wapi mpaka mafundi wetu wafuatilie na kufika katika eneo husika, lakini kituo hiki kitatuwezesha kutumia mfumo wa kompyuta kuonyesha eneo lenye kasoro.”
Habari zaidi soma Jarida la Uchumi ndani.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop