Welcome to our online store Portal

Template Information

Tuesday, February 25, 2014

MTANZANIA MMOJA AKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA KETE 71

http://azizicompdoc.blogspot.com/

Polisi Kikosi cha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), wamemkamata mkazi wa Temeke, Mwanahamisi Salim (27) kwa tuhuma za kumeza kete 71 za dawa za kulevya aina ya heroini zenye thamani ya zaidi ya Sh60 milioni.
Mkuu wa Upelelezi wa Viwanja vya Ndege Tanzania, Hamad Hamad alisema mtuhumiwa huyo alikamatwa alasiri ya Februari 20, mwaka huu akijiandaa kupanda Ndege ya Shirika la Emirates kwenda Hong Kong, China.
“Tulipomhoji alitueleza kuwa dawa hizo alikuwa anazipeleka kwa marafiki zake kutoka Nigeria ambao wanaishi Hong Kong lakini bado tunaendelea kumhoji ametoa wapi huo mzigo,” alisema Hamad.
Alisema katika siku za karibuni, wamebaini kuwa watuhumiwa wengi wanaokamatwa ni wanawake.
Alisema wengi wa wanawake hao wanadai wanakwenda kununua vifaa vya saluni.
Kamanda wa Polisi, Kitengo cha Kupambana na Dawa za Kulevya, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP), Godfrey Nzowa alisema dawa zilizokamatwa ni heroini.

Katika hatua nyingine; taswira ya Tanzania imeendelea kuchafuka baada ya Kituo cha Kimataifa cha Televisheni cha France 24 kutoa ripoti inayoonyesha ukubwa wa tatizo la dawa za kulevya nchini.
Ripoti hiyo inakuja zikiwa zimepita wiki mbili tangu Gazeti la The Mail on Sunday kuandika habari za kukithiri kwa ujangili wa meno ya tembo na pembe za faru.
Taarifa ya kituo hicho ilieleza kuwa Tanzania inaonekana kuwa kituo cha dawa za kulevya kutoka Afghanistan na Pakistan.
Mmoja wa waandishi walioandaa ripoti hiyo, Jaouhar Nadi alisema tatizo la dawa za kulevya Tanzania ni kubwa na hakuna mikakati ya makusudi ya kupambana nalo.
“Zanzibar kwa mfano, kuna watumiaji 10,000 wa dawa za kulevya, yaani katika kila familia moja kuna mteja mmoja. Kuna ‘mateja’ wapatao 250,000 nchi nzima na jitihada za Serikali zinaonekana kuwa dhaifu,” alisema Nadi alipokuwa akihojiwa na France 24 na kuongeza: “Zanzibar kwa mfano, hakuna programu yoyote ya Serikali zaidi ya ile iliyoanzishwa na taasisi ya Kimarekani.”

Nadi alisema licha ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano kuanzisha Tume ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, bado uingizwaji wa dawa hizo umekithiri.
“Mamlaka zinashughulikia suala hilo, walianzisha tume miaka ya 1990. Hata hivyo, usafirishaji wa dawa za kulevya bado ni mkubwa,” alisema na kuongeza:
“Inakadiriwa kuwa biashara hiyo huingiza zaidi ya Dola 165 milioni na tani 22 za heroini huingizwa nchini humo kila mwaka. Hizo ni fedha nyingi na watu wanaamini kuna rushwa hasa kwa viongozi wa juu na wabunge.
“Majina ya wakubwa wanaohusika na biashara hiyo yanafichwa. Wengi wanaamini ni kazi ya wafanyabiashara wakubwa wa dawa hizo.”

Akizungumzia madai hayo Kamanda Nzowa alipinga utafiti huo na kusema jitihada kubwa zimefanyika... “Kama ni kweli kuna tatizo kubwa kiasi hicho, hao waandishi walipaswa watuambie dawa hizo zinauzwa bei gani, kwa sababu ninavyojua ni kwamba, huko mitaani dawa zinauzwa bei ghali mno. Kilo moja inafikia hadi Sh50 milioni, sasa utasemaje kwamba matumizi ya dawa yameongezeka?”
“Ni kweli tatizo la dawa za kulevya lipo, pia ukamataji ni mkubwa. Kwa mfano, mwaka jana tu tumekamata kilo 1,882 za heroini. Februari 4, mwaka huu tumekamata kilo 201 na wenzetu wanaodhibiti baharini wamekamata kilo 350 za dawa hizo. Hiyo pekee inajenga hofu kwa waingizaji. Itakuwaje waendelee kuleta?”
Alisema majina ya watu wanaohisiwa yamekuwa yakifanyiwa kazi ikiwa pamoja na kuwafikisha mahakamani... “Mwaka jana kuna gazeti moja la Kiswahili lilifanya utafiti na mimi pia nilizungumza nao. Baada ya hapo tulikamata watu 266. Baada ya kuwapekua hatukuwakuta na ushahidi, lakini bado tuliwafikisha mahakamani kwa kuwa walikuwa na dalili za kuhusika,” alisema na kuongeza:
“Tunapata taarifa mbalimbali na tunawashukuru wananchi, lakini wanapaswa watupe kwa siri siyo kutangaza hadi wahusika washtuke. Hii ni vita ya dunia nzima, siyo Tanzania tu.”
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Zanzibar, Mohamed Aboud alisema hana taarifa za kutosha kuhusu utafiti huo, lakini hali siyo mbaya kiasi hicho.
“Ni kweli kuna tatizo la dawa za kulevya hapa Zanzibar na watu wengi wameathirika, lakini sidhani kama ni kwa kiasi kikubwa hivyo. Bado tunafuatilia utafiti huo ili kujiridhisha na kutoa taarifa rasmi,” alisema Aboud.

Related Product :

0 comments:

Post a Comment

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop