Taarifa kutoka hapa mahakama kuu Dar ni kwamba Zitto Kabwe ameshinda kesi dhidi ya Chadema, wafuasi wa Zitto wamejawa na furaha kupita kiasi
Kwa mantiki hiyo Zitto amepewa kinga na mahakama hiyo, hivyo Chadema haitamjadili kwa namna yoyote ile
Ikumbukwe kuwa leo macho na maskio ya watanzania hasa wafuasi na wapenzi wa CHADEMA yalielekezwa katika Mahakama Kuu
Kanda ya Dar es Salaam,pale ambapo Jaji wa Mahakama hiyo Jaji John
Utumwa alikuwa akitoa hukumu dhidi ya Zitto Kabwe na CHADEMA....
Zitto ambaye alikuwa ni Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho, alifungua kesi
katika Mahakama hiyo akipinga hatua ya Kamati Kuu ya Chama hicho iliyokutana tarehe 3 na 4 mwezi huu
kujadili hatima ya uanachama wake wakati baraza kuu halijakaa na kujadili rufaa yake...
Akisoma hukumu ya kesi hiyo baada ya kuiahirisha jana, Jaji wa mahakama hiyo,Jaji
Utamwa ameridhia pingamizi lililotolewa na mh. Zitto Kabwe la
kutojadili uanachama wake na kuitaka kamati kuu ya CHADEMA au
chombo kingine chochote kisijadili uanachama wake hadi kesi
yake ya msingi ( rufaa ) itakaposikilizwa na baraza kuu la
chama hicho.
Mh
Zitto
Kabwe (kulia) akitoka katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Dar es Salaam
leo, ambapo aliwasilisha ombi la pingamizi la yeye kutojadiliwa kwenye
kikao cha Kamati Kuu ya chama hicho kinachotarajia kufanyika kesho, hadi
rufaa yake ya kupinga kuenguliwa wadhifa huo kwenye Baraza Kuu la chama
hicho. Kushoto ni Wakili wa Zitto, Albert Msando. Mahakama Kuu
imekubaliana na Zitto Kikao cha Kamati Kuu ya Chadema kinachotarajiwa
kufanyika kesho kutomjadili kwa namna yoyote.
Zitto Kabwe akiingia mahakama Kuu Dar es Salaam leo
Wanasheria wa Chadema, Tundu Lisu (kushoto) na Peter Kibatala waliofika kupinga hoja hiyo mahakamani.
Tundu Lisu na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema wakijadiliana jambo wakati wakisubiri uamuzi wa mahakama
Zitto
ana wakili wake Msando wakiwasiliana na marafiki zao walipokuwa
wakisubiri uamuzi wa mahakama, ambapo Zitto aliibuka kidedea kwa pingamizi
lake kukubaliwa hivyo kikao cha Kamati Kuu kinachofanyika kesho
kukatazwa kumjadili kwa namna yoyote Zitto.
hapa umeweka kiporo kwenye friji na kitaliwa tu kama sio nawewe kitaliwa na watoto
ReplyDelete