Welcome to our online store Portal

Template Information

Wednesday, July 31, 2013

MAMLAKA YA MKOA WA LINDI YATOA RASMI ENEO KWA AJILI YA UJENZI WA CHUO KIKUU

Ufuatiliaji wa jengo na eneo kwa dhumuni la kujenga chuo kikuu huria cha Tanzania kwa mkoa wa lindi uliofanywa na mzawa wa lindi Bw Abdulazizi Mnyengema kuanzia tar 05/03/2013 mpaka tar 14/03/2013 ktk mamlaka ya mkoa wa Lindi umezaa matunda baada ya viongozi wa mkoa huo kukubali ombi hilo la mzawa huyo kupitia ofisi yake ya chuo kikuu huria cha Tanzania lindi.

Mamlaka ya mkoa wa Lindi imeamua kuzidi kuuendeleza mkoa huo kwa kuamua kukubali ombi la Chuo kikuu huria cha Tanzania kulichukua eneo lisiloendelezwa kwa muda mrefu na kujenga jengo kubwa la chuo hicho na kuwanufaisha wananchi wa Lindi na Watanzania kwa ujumla.

Kutokana na maamuzi hayo, Chuo kikuu huria kitaanda mapokezi ya eneo hilo kutoka kwa Mamlaka ya mkoa na kukabizi gari mpya aina ya TATA kibini mbili (Doble cabin) yenye no za usajili SU 39761 ambayo itatumika kuchochea maendeleo ya chuo na mkoa kwa ujumla.
Wanalindi wajiandae kupokea na kuzitumia fursa hizi adimu na kuzidi kuwaunga mkono kila wenye nia nzuri na lindi.
Lililokua Ghala la kampuni ya usagishaji la Taifa (NMC) lililoridhiwa na mkoa kupewa Chuo kikuu huria cha Tanzania kwa uendelezaji.
Gari mpya iliyonunuliwa kwa ajili ya chuo kikuu huria Lindi

Eneo la ghala hilo kwa ndani

Eneo la ghala hilo kwa ndani

Gari hiyo mpya kwa ubavuni iliyonunuliwa kwa ajili ya chuo kikuu huria Lindi

View detail

Saturday, July 27, 2013

MAUAJI MAKUBWA WAYAFANYA MAJESHI YA MISRI

Wafuasi wa rais wa Misri aliyeondolewa madarakani na jeshi,Mohamed Morsi wamesema zaidi ya watu laki moja na ishirini wameuwawa katika mapambano na vikosi vya ulinzi na usalama mjini Cairo.
Polisi waliingia katika mkusanyiko wa usiku wa wafuasi wa Morsi saa chache baada ya waziri wa mambo ya ndani kusema wafausi wa Morsi na chama chao cha Muslim Brotherhood waliokusanyika kwenye viunga vya msikitini wa Rabba Al Adawiya lazima waondoke.

Muslim Brotherhood wamelilaumu jeshi kwa kuwapiga risasi na kuwauwa wafuasi wao.
Daktari katika hospitali ya muda amesema watu wawili walifikishwa wakiwa kichwa na viwili wili vyao vimetenganishwa huku wengine wakiwa na matundu ya risasi vichwani na kifuani.
Hospitali hiyo imekuwa katika hali ngumu ya kumudu miili ya marehemu na majeruhi wanaofikishwa hospitalini hapo.
Mwandishi wa azizicompdoc.blogspot.com anasema ni mapigano mabaya zaidi tangu jeshi limuondoe rais Morsi madarakani.

Wakati huo huo, Uingereza imekemea matumizi ya nguvu yanayopoteza maisha ya watu nchini Misri.
Waziri wa masuala ya kigeni William Hague amewataka wenye mamlaka kumaliza mapigano na vurugu hizo.
Amesema wale waliohusika na mauaji hayo ni lazima wawajibike na haki ya wanaoandamana kwa amani ni wajibu ilindwe.
Bwana Hague pia amelitaka jeshi kuwachilia huru viongozi wa Muslim Brotherhood waliowekwa kizuizini akiwemo rais Mohamed Morsi. View detail

AFUKUZWA KANISANI KWA KUVAA NUSU UCHI!

Wakati mwanamke wa kivazi kilichositisha ndoa kanisani kwa dakika kadhaa akidai hakuwa na tatizo kuvaa vile, Katekista wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Peter, Yohane Maboko, amesisitiza kuwa alikiuka maadili ya Kanisa.
Mwanamke huyo ambaye ameendelea kukataa kutaja jina lake, huku njia zingine zikimtaja kwa jina la Restituta Kalemera, alidai juzi kuwa kivazi hicho cha mabega wazi hakikuwa tatizo kanisani, bali ni unyanyasaji tu wa Katekista huyo.

Akizungumza  juzi, alidai kuwa Katekista Maboko alimsukuma na kumwangusha katika ngazi ndefu za Kanisa hilo lililoko Oysterbay, Dar es Salaam.

"Wakati Katekista akinitaka nitoke nje, ghafla alinisukuma nikaanguka kwenye ngazi na kudakwa na mtu mwingine aliyeniokoa, la sivyo ningeumia vibaya," alidai.


Alidai kilichomsikitisha ni kudaiwa kutaka kuingia kanisani akiwa amevaa nguo zilizoacha mwili wazi, jambo ambalo si la kweli, kwa kuwa alikwenda kanisani hapo akiwa na kitambaa kilichofunika mwili.

"Nilipofika kanisani, nilikutana na Katekista akimrudisha mtu mwingine, ghafla alitokea bibi harusi aliyevalia nguo ambazo hazikuruhusiwa kanisani, akaniomba skafu niliyokuwa nayo, nikampa nami kubaki wazi mabegani," alidai.

Baada ya kuvua kitambaa hicho, alidai alitaka kuingia kanisani ili kuchukua funguo za gari, lakini alikutana na Katekista kwenye ngazi, ambaye alimwamuru atoke nje naye akaendelea kumsihi kuwa anakwenda kuchukua funguo za gari ndani, hata hivyo hawakukubaliana.


Aliendelea kudai, kuwa Katekista alipomsukuma na kuanguka, baada ya kudakwa alichanganyikiwa akidhani kanisani ni sehemu ya malumbano, akakimbilia ndani kutafakari, huku kiatu chake alichonunua nje ya nchi (Uingereza) kikiwa kimeharibika.

Alidai kuwa akiwa kanisani, Katekista alimfuata tena na kumsihi atoke nje, jambo lililosababisha ndugu zake wamzingire kiongozi huyo wa Kanisa na kumhoji kwa jazba, sababu ya kumsukuma ndugu yao na kuhatarisha maisha yake.

Baada ya malumbano huyo, alitoka nje ya Kanisa na kuacha utaratibu mwingine ukiendelea, huku akilalamika kwamba Kanisa ni sehemu takatifu hivyo hapatakiwi kuwa uwanja wa mapigano na kwamba limeacha kazi ya kufundisha na kuomba ielezwe wazi watu wavae nini.


Akijibu tuhuma hizo, Katekista Maboko alimpongeza mwandishi kwa kushuhudia tukio hilo na kutoa habari yake na kuongeza kuwa utaratibu wa jinsi ya kuingia kanisani kwa maharusi, umekuwa ukifundishwa tangu kuandikishwa kwa ndoa hadi mafundisho ya ndoa.

Alisema dada huyo alipofika kanisani hapo, alikuwa na wanawe wawili waliokuwa na mavazi yaliyoacha sehemu za miili yao wazi, na aliwaelewesha lakini yeye akabisha.

"Niliwashika mikono na kuwapeleka uliko ubao ili wasome maelekezo ya kinachotakiwa kuvaliwa, lakini yeye alilazimisha kuingia huku akisema Mungu haangalii mavazi, bali roho," alisema Katekista Maboko na kuongeza kuwa wakati akieleza hayo, ndipo wanandugu walipofika na kumhoji.


Kuhusu miwani yake kuvunjwa, alisema wakati akiwa amezungukwa na watu kama 30 kwa lengo la kumchanganya, aliendelea kujenga hoja kuwa kanisani zipo taratibu zinazotakiwa kuzingatiwa, lakini mmoja wao alitumia nguvu na kuvunja miwani hiyo.

Hata hivyo, alisema mtu huyo aliomba samahani na kulipa kiasi cha fedha, ambapo walipeana mikono kama ishara ya kusameheana.

Katekista Maboko alisema kwa ufupi kilichotokea, ni kukosekana kwa busara kwa waumini hao, kwani vipo vibao vinavyotoa maelekezo juu ya utaratibu unaotakiwa na unaopaswa kufuatwa
View detail

Tuesday, July 16, 2013

CHADEMA KUFUTWA KAMA HAKITAFUATA MAAGIZO YA SERIKALI


Ofisi ya msajili wa vyama vya siasa chini ya mwenyekiti wake Bwana John Tendwa imesema imesikitishwa na Chama cha CHADEMA kuanzisha kambi za mafunzo ya ulinzi (Red Brigade).
Ofisi hiyo ya msajili imekitaka chama cha CHADEMA kuachana na mpango wa mafunzo ya vikundi mara moja vinginevyo ofisi hiyo itakichukulia hatua kali, na hatua hiyo ni kukifutia usajili moja kwa moja chama hicho cha siasa.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari imewataka wale wote wanaosema kuwa CCM inavyo vikundi vya ulinzi, wapeleke ushahidi huo na wao kama wasajili wa vyama vya siasa watakifungia bila kusita. View detail

Ghasia zaendeleamjini Cairo Misri huku Watu 7 wakiripotiwa kuuwawa

Ghasia zimekuwa jambo la kila mara Misri tangu Morsi kuondolewa mamlakani

Watu saba wameuawa mjini Cairo usiku wa kuamkia leo kufuatia makabiliano makali kati ta wanajeshi wa serikali na wafuasi wa rais wa Misri aliyeondolewa madarakani, Mohamed Morsi.
Polisi walitumia vitoa machozi kuwatawanya na kuwasukuma nyuma waandamanaji hao ambao walikuwa wakiwarushia mawe huku wakiwa wamefunga barabara kuu inayoelekea kati kati mwa mji mkuu.
Ghasia hizo zimetokea huku naibu waziri wa mambo ya nje wa Marekani, William Burns akiwa ziarani nchini humo.
Waziri huyo amesema taifa hilo limepewa nafasi ya pili kurejesha utawala wa kidemokrasia.
Bwana Burn alifanya mashauriano na viongozi wa serikali ya mpito ya nchi hiyo, lakini viongozi wa chama cha Muslim Brotherhood, walisusia mkutano huo.
Awali mamia ya wafuasi wa kiongozi aliyepinduliwa Misri Mohamed Morsi wamepambana na vikosi vya usalama katikati mwa mji wa Cairo na kuwafyatulia waandamanaji hao gesi ya kutoa machozi.
Mapigano hayo yanajiri muda mfupi baada ya mjumbe mkuu wa Marekani William Burns kutoa wito kwa vikosi vya usalama kujizuia kwa kiwango kikubwa katika kukabiliana na maandamano hayo.
Makabiliano yalifanyika baada ya naibu waziri wa mambo ya nje wa Marekani anayezuru Misri, kuwataka maafisa wa usalama kuhakikisha kuwa wanajitahidi kutuliza ghasia wakati wakijizuia kufanya mauaji yoyote.
Burns alikutana na maafisa wa serikali inayoungwa mkono na majeshi.
Lakini chama cha Muslim Brotherhood kimesema haikina nia ya kukutana na waziri huyo.
Akizungumza baada ya kukutana na viongozi wa serikali mpya inayoungwa mkono na jeshi nchini, mjumbe huyo, William Burns, amesema Misri imepewa nafasi ya pili kufuatia kupinduliwa na jeshi Mohammed Morsi.
Alikutana na serikali inayoungwa mkono na jeshi nchini lakini Muslim Brotherhood, inasema haina mpango wa kukutana naye. Naibu rais wa tawi la kisiasa la chama cha Morsi, Muslim Brotherhood,Essam el-Erian, ametoa wito wa utulivu.
View detail

Sunday, July 14, 2013

ASKARI 7 WA TANZANIA WADAIWA WAMEUAWA DARFUR KTK KIKOSI CHA UMOJA WA MATAIFA CHA KULINDA AMANI


Dar es Salaam. Wanajeshi saba wa Tanzania, ambao ni miongoni mwa kikosi cha Umoja wa Mataifa, cha kulinda amani katika jimbo la Darfur nchini Sudan, wanadaiwa kuwa wameuawa.
Taarifa zilizoifikia Blog hili jana zilisema kwamba wanajeshi hao wa Tanzania, wamekufa kutokana na mashambulizi yaliyofanywa na waasi wanaopigana na Serikali.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, miili yao wanajeshi hao bado ipo nchini Sudan ikisubiri taratibu za kusafirishwa kuletwa nchini.
Hii ni mara ya kwanza kuripotiwa kwa idadi kubwa ya wanajeshi wa Tanzania wanaolinda amani katika nchi mbalimbali kufa kwa wakati mmoja.
Agosti mwaka jana wanajeshi watatu wa Tanzania huko Darfur waliripotiwa kuuawa kwenye tukio kama hilo.
Msemaji wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) , Kanali Kapambala Mgawe alipoulizwa kwa njia ya simu kuhusu vifo vya wanajeshi wa Tanzania huko Darfur, alisema kuwa naye amesikia, lakini hana taarifa rasmi kwa mujibu wa taratibu za kiofisi.
Hii ni mara ya pili kwa wanajeshi wa Tanzania kuuawa katika Jimbo la Darfur, ambapo Agosti mwaka jana, Kanali Mgawe alinukuliwa na vyombo vya habari akithibitisha kutokea kwa vifo vya askari watatu ambao gari lao lilizolewa na maji walipokuwa wakivuka mto uliokuwa umefurika maji.
Kanali Mgawe aliwataja askari hao kuwa ni Sajini Julius Chacha, Sajini Anthony Daniel na Koplo Yusuph Said na kwamba askari wengine walinusurika baada ya kuogolea.
Tanzania ina askari 850 kwenye kikosi cha Umoja wa Mataifa cha Kulinda Amani jimbo la Darfur, ambao ni sehemu ya askari 1,081 wa kulinda amani katika jimbo la Darfur.
Wanajeshi hao wa Tanzania wametawanywa kwenye miji ya Khor Abeche na Muhajeria kusini mwa Darfur.
Aprili mwaka huu Tanzania ilipeleka wanajeshi wa kulinda amani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), kupambana na kikundi cha waasi wa nchi hiyo M23 kinachopigana kuiangusha serikali ya DRC.
Majeshi ya Tanzania yalipelekwa kulinda amani chini ya Umoja wa Mataifa. Tanzania inaungana na nchi za Afrika Kusini na Malawi kukamilisha kikosi cha wanajeshi 3,000. Tanzania imepeleka wanajeshi 850.
View detail

WAFUASI WA MORSI WAJITOA MUHANGA, CAIRO MISRI HAKUKALIKI



Wafuasi wa rais wa zamani wa Misri Mohamed Morsi

Wafuasi wa rais wa Misri aliyeondolewa madarakani Mohammed Morsi wamefanya maandamano makubwa mjini Cairo, huku waumini wa dini ya Kiislamu wakiadhimsiha Ijumaa ya kwanza tangu kuanza kwa mwezi mtukufu wa Ramadan.
Wafuasi wa kiongozi huyo wa vugu vugu la Muslim Brotherhood walijikusanya Mashariki mwa mji huo, kushinikiza utawala wa kijeshi kumrejesha madarakani kiongozi wao.
Wapinzani wa rais huyo wa zamani ambao waliandamana hadi rais huyo akaondolewa madarakani na jeshi watakusanyika katika medani ya Tahrir.
Watu kadhaa wameuawa kwenye ghasia zilizotokea tangu Morsi alipoondolewa.
Mwandishi wa www.azizicompdoc.blogspot.com mjini Cairo,  anasema vuguvugu la Muslim Brotherhood huenda liliwatenga raia wengi wakati wa utawala wa Morsi, lakini bado raia wengi wa nchi hiyo hawataki jeshi kuingilia masuala ya siasa.

Marekani kutuma ndege za kivita Misri

Siku ya Alhamisi serikali ya Marekani, ilitoa wito kwa utawala mpya wa Misri, kusitisha harakati zake za kuwakamata wanachama wa vuguvugu la Muslim Brotherhood na kuonya dhidi ya kulenga kundi lolote.
Wanajeshi wakishika doria mjini Cairo
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon vile vile ameonya utawala huo wa Misri kutotenga chama chochote cha kisiasa katika harakati za kutatua mzozo wa kisiasa unaokumba taifa hilo.
Hata hivyo msemaji wa Ikulu ya White House, Jay Carney amesema, utawala wa Washington hauamini kuwa ni lazima isitishe misaada yake ya Misri.
Marekani inatarajiwa kupeleka ndege nne za kivita aina ya F-16 nchini Misri, lakini haijathibitisha kuwa msaada huo utatolewa lini.
Serikali ya Marekani imesema, inachunguza ikiwa aumuzi huo wa jeshi la Misri kumuondoa madarakani rais Morsi ni mapinduzi ya Kijeshi kwa kuwa sheria za Marekani inazuia serikali kutoa misaada kwa nchi yoyote ambayo kiongozi aliyechaguliwa kwa njia ya kidemokrasia ataondolewa kupitia mapinduzi.
Wafuasi wa rais Morsi wamekuwa wakiandamana wiki nzima karibu na kambi ya kijeshi iliyoko Mashariki mwa mji mkuu wa Cairo, ambako wanaamini kuwa kiongozi wao anazuiliwa na maafisa wa kijeshi tangu alipoondolewa madarakani.
View detail

Tuesday, July 9, 2013

SOKO KUBWA LAWAKA MOTO MOGADISHU


Gari limelipuka ndani ya soko rasmi mjini Mogadishu nchini Somalia.
Kwa mujibu wa polisi, hakuna taarifa zaidi kuhusu waliojeruhiwa katika shambulizi hilo kwenye soko la Bakara.
Walioshuhudia shambulizi wanasema kuwa gari lilikuwa limewabeba watu waliokuwa wamevelia magwanda ya jeshi.
Hakuna kundi lolote limekiri kufanya shambulizi hilo, lakini kundi la wapiganaji wa kiisilamu wa al-Shabab, limekuwa likifanya mashambulizi ya kuvizia tangu kuondolewa kutoka mjini Mogadishu mwaka 2011.
Polisi walifahamisha azizicompdoc.blogspot.com kuwa afisaa mkuu wa polisi amejeruhiwa kwenye shambulizi hilo, lakini hakuna taarifa zaidi hadi uchunguzi utakapokamilika.
Afisaa wa polisi Mohamed Hussein, alisema bomu lilikuwa limefichwa ndani ya gari la kijeshi, na limewajeruhi wanajeshi watano wa serikali.
Naye Hussein Nur, ambaye ni mfanyabiashara wa pesa, alisema alishuhudia gari likilipuka.
Kundi la Al-Shabab linapigana likitaka kuruhusiwa utawala wa kiisilamu nchini Somalia na licha ya kufurushwa kutoka mji mkuu Mogadishu katika miaka miwili iliyopita,lingali linadhibiti sehemu kubwa ya nchi.
Wanajeshi 18,000 wa Afrika, wako nchini Somalia kuunga mkono serikali ya Somalia iliyo chini ya rais Hassan Sheikh Mohamud, aliyechaguliwa na wabunge mwaka jana. View detail

Thursday, July 4, 2013

BAKHRESA AIONYESHA SERIKALI KUA ANAWEZA BILA KUWEZESHWA

Eneo la mapokezi ya abiria linavyoonekana kwa nje lililojengwa Zanzibar kwa ufadhili wa Bakhresa
 Tajiri nambari moja Tanzania na wa 30 Afrika  Said Salim Bakhesa ameidhihirishia Serikali ya Tanzania kua ana uwezo wa kufanya mabadiliko makubwa ktk nchi yake kwa kuamua kuliendeleza eneo la bandari ya Zanzibar kutokana na serikali hiyo kushindwa kuliendeleza eneo hilo kutokana na hali ya kifedha kua mbaya na kuamua kumkabizi mfanya biashara huyo mkubwa Tanzania na Afrika na kweli ameonyesha anaweza,
Ufadhili huo ni pamoja na Jengo kwa ajili ya watu wa TRA, Mamlaka ya Bandari ZNZ, Polisi, Uhamiaji maduka na ofisi mbalimbali kwa matumizi ya serikali. Kwa kweli serikali ilifanya uamuzi wa busara kumkabizi mzawa bandari hii na hatuna budi kuiunga serikali mkono kwa hili na kujitahidi kumuamini zaidi mzawa kuliko wawekezaji wanaohamisha mali zetu kila kukicha na kutuacha tukiwa duni kila siku.

Eneo la Bandari ya Zanzibar linavyoonekana kwa nje lililojengwa Zanzibar kwa ufadhili wa Bakhresa

Eneo la kupumzikia abiria lililopo bandari ya zanzibar kwa ufadhili wa Bakhresa

View detail

Tuesday, July 2, 2013

OBAMA AFANYA VIHOJA TANZANIA YABAKIA KUA GUMZO NCHINI

RAIS OBAMA AMALIZA ZIARA YAKE NCHINI TANZANIA MCHANA HUU

 
RAIS Barack Obama wa Marekani ameondoka nchini mchana huu kurudi nchini Marekani,baada ya kumaliza ziara yake ya siku mbili hapa nchini iliyoanza jana.
 
 
Rais Obama na mwenyeji wake Rais Jakaka Kikwete, leo walifanya ziara ya kutembelea mitambo ya kuzalisha umeme ya Symbion iliopo Ubungo jijini Dar es Salaam na kuzindua rasmi mradi huo.
Tunapenda  kuungana na  Rais Jakaya  Kikwete na  watanzania  wote  wapenda amani katika  kumshukuru Rais wa Marekani Barack Obama kwa  kuichagua  Tanzania.

Pia tunawapongeza  watanzania  wote kwa kuonyesha umoja  wetu na hata  kuzika itikadi zetu za kisiasa   na   hata  kupelekea  TV zaidi ya 1000 duniani na radio zaidi ya  3000 duniani  kuitazama  Tanzania. 



View detail

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop