Welcome to our online store Portal

Template Information

Thursday, January 31, 2013

Dr. Asha-Rose Migiro ateuliwa kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania





View detail

Wednesday, January 30, 2013

PINDA APOZA HASIRA ZA WANA MTWARA. KIWANDA CHA KUCHAKATA GESI SASA LAZIMA KIWE MTWARA


Waziri mkuu, Mizengo Pinda amefanikiwa kutuliza jazba za wakazi wa Mkoa wa Mtwara baada ya kueleza jinsi watakavyonufaika na gesi itakayozalishwa mkoani humo kabla ya kusafirishwa kwa bomba hadi Dar es Salaam.






Aidha, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Joseph Simbakalia amewaomba radhi wananchi wa mkoa huo kutokana na kauli Desemba 21, mwaka jana akiwakebehi baada ya kumwomba apokee maandamano yao ya kupinga mpango wa kusafirisha gesi hiyo.
Akizungumza katika mkutano wa majumuisho uliofanyika jana baada ya kusikiliza madai ya wananchi hao kwa siku mbili mfululizo, Pinda alisema hakuna tone la gesi ghafi itakayosafirisha kwa njia ya bomba na kusema kiwanda cha kusindika gesi ghafi kitajengwa katika Kijiji cha Madimba, mkoani humo ili mabaki yatokanayo na gesi hiyo yatumike kuvutia uwekezaji wa viwanda.
“Wataalamu wanasema gesi haiwezi kwa namna yoyote ile kusafirishwa kama ilivyo, lazima ibadilishwe kuwa hewa au barafu… kiwanda cha kusafisha gesi kitajengwa Madimba. Gesi yote itakayotoka Mnazi Bay itasafishwa hapo na masalia yote yatabaki huku ili kuvutia viwanda vya mbolea na vingine vinavyotumia malighafi hizo,” alisema Pinda na kuongeza:
“Kama tungekuwa tunasafirisha gesi ghafi basi hata kiwanda cha Dangote kisingejengwa hapa… gesi itakayopelekwa Dar es Salaam ni ile iliyosafishwa kwa ajili ya matumizi ya kuzalisha umeme… tusaidieni wenzetu kuliokoa Taifa na tatizo la umeme.”
“Gesi lazima isindikwe Mtwara, haitoki hadi viwanda vije… nadhani hili ni jambo jema lazima tuliwekee utaratibu. Nikawauliza wataalamu wangu kwani kiwanda cha kusafisha gesi kinajengwa wapi, wakanijibu Madimba… nikasema kumbe tatizo kubwa ni kutowaeleza vya kutosha wananchi suala la gesi.” alisema Waziri Mkuu huku akipigiwa makofi... “Nafikiri tatizo ni sisi Serikali hatukuwa na mpango mzuri wa kuwaelimisha wananchi.”
Awali, madai ya wakazi wa Mkoa wa Mtwara yalikuwa ku pinga usafirishaji wa gesi ghafi kwenda Dar es Salaam wakieleza kuwa mpango huo utafukuza uwekezaji wa viwanda mkoani humo ambao ungechochewa na upatikanaji wa malighafi baada ya kusafishwa kwa gesi.
Pia wananchi walipinga uje nzi wa mitambo ya kuzalisha umeme Kinyerezi, Dar es Salaam wakiitaka Serikali kujenga mitambo hiyo mkoani Mtwara.
Alitoa wito kwa wabunge wa Mkoa wa Mtwara kufuta tofauti zao za kisiasa ili waweze kuharakisha maendeleo ya mkoa huo... “Purukushani hizi ndani ya chama hazina tija, tuseme basi… wabunge hawaelewani, sasa bungeni wanakwendaje... kila mtu na lake … hebu tuseme watu kwanza mimi badaaye,” alisema Pinda huku akishangiliwa.
Katika siku hizo mbili mkoani Mtwara, Waziri Mkuu alikutana na viongozi wa vyama vya siasa, dini, wafanyabiashara, madiwani na wenyeviti wa mitaa na wanaharakati mbalimbali.

MKUU WA MKOA WA MTWARA AOMBA RADHI MBELE YA HADHRA KWA KAULI ZAKE
Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa, Simbakalia aliwaomba radhi wakazi wa Mkoa wa Mtwara akisema alipotoka kuwaita wananchi hao wapuuzi na baadaye wahaini kauli ambazo ziliwaudhi wengi
“Kupitia hadhara hii nawaomba radhi kwa kuwakwaza, nimesikitishwa kwa kauli yangu ambayo imepokewa kwa hisia kwamba niliwadharau,” alisema Simbakalia.
Baadaye Waziri Mkuu aliwasihi wananchi wa Mtwara kumsamehe Mkuu wao wa Mkoa wa Mtwara kwa kauli hiyo aliyoitoa 21 Desemba, mwaka jana katika kikao cha Kamati ya Ushauri Mkoa, (RCC), pale alipoombwa kuyapokea maandamano ya wakazi wa mkoa huo Desemba, 27, mwaka jana.
View detail

Monday, January 28, 2013

Upinzani wakataa mazungumzo Misri

Serikali ya rais Morsi inakabiliwa na upinzani mkali


Kundi kubwa zaidi la upinzani nchini Misri limesema halitahudhuria mazungumzo yanayoandaliwa na Rais Mohamed Morsi hadi pale masharti yatakapotimizwa.
Mkutano huo ulinuia kumaliza machafuko ambayo yamekuwa yakiendelea katika miji kadhaa katika siku za hivi karibuni.
Awali Rais Morsey alitangaza hali ya hatari ya muda wa mwezi mzima katika miji ya Port Said, Suez na Ismailiya kufuatia siku kadhaa ya maandamano na fujo.
Amesema kuwa pia ameweka amri ya kutotoka nje usiku kucha. Kiongozi wa kundi la upinzani la Free Egyptians Party, Dr Ahmed Saeed, ameaimbia azizicompdoc.blogspot.com kuwa rais Mosri anapaswa kufanya juhudi zaidi kurejesha imani ya wananchi.
Mapema leo Rais wa Misri Mohammed Morsi ametangaza hali ya tahadhari katika miji ya Port Said, Suez na Ismalia baada ya siku kadhaa za machafuko makali.
Kuanzia Jumatatu na kwa siku 30 zijazo watu hawatakubaliwa kutoka nje kati ya saa 21:00 na 06:00, alisema alipohutubia taifa.
"Huwa kwa kawaida napinga hali za tahadhari, lakini ilibidi niwalinde wananchi na kukomesha umwagikaji damu basi ikanabidi nifanye hivyo,” rais alisema.
Takriban watu 33 people walikufa mnamo wikiendi huko Port Said, ambapo uamuzi wa mahakama ulisababisha vurugu kuzuka.
Kutoridhika na uongozi wa Bwana Morsi's kulizua fujo kwingine nchini.
Katika mji mkuu wa Cairo, waadamanaji wailokuwa wanaipinga serikali walipambana na vikosi vya ulinzi karibu Uwanja wa Tahrir kwa siku ya nne mfululizo.
Upinzani unamlaumu Morsi kwa kutawala kimabavu na kuipa kipaumbele katiba mpya ambayo hailindi kikamilfu haki za kuabudu wala za maoni.
Serikali pia imelaumiwa kwa kutodhibiti hali ya uchumi, inayozidi kuzorota.
Bwana Morsi alisema kwamba angechukua hatua zaidi "kwa ajili ya Misri" na kwamba ilikuwa "wajibu wake" kama rais kufanya hivyo.
Vuru katika mji wa Portland

Aidha, aliwaalika viongozi wa kisiasa wakutane "katika majadiliano ya kitaifa " mnamo Jumatatu.
Ingawaje muungano mkubwa zaidi wa vyama pinzani nchini Misri, National Salvation Front, uliuunga mkono mualiko huo, ulilaumu sera za Morsi kwa kuzua vurugu.
Vurugu zilizuka Port Said baada ya mahakama kuwahukumu watu 21 kifo kwa kuhusika na fujo baada ya mechi ya kandanda Februari 2012.
View detail

Saturday, January 26, 2013

Ofisi ya serikali yachomwa moto Suez




Hayo yametokea wakati maelfu ya watu wakipita mabara-barani kwenye mhadhara wa mazishi ya wale waliokufa katika mapambano ya Ijumaa - siku ya kuadhimisha miaka miwili ya kuanza ghasia zilizomuangusha Rais Hosni Mubarak.
Wanajeshi wa serikali wanaendelea kupiga doria mjini Suez.
Watu kama 10 walikufa katika ghasia za Ijumaa.
Mjini Cairo, mapambano piya yamezuka kati ya askari polisi na waandamanaji karibu na wizara ya mambo ya ndani ya nchi ya Misri.
Polisi walifyatua moshi wa kutoza machozi kujaribu kuwazuwia waandamanaji wasifike kwenye jengo la wizara.
View detail

COMPUTER DOCTOR YASHIRIKIANA NA UTUMISHI KUKULETEA AJIRA KARIBU. BOFYA PICHA HII UONE KAZI ZILIZOPO KWA SASA

MASASI KWAZIDI KUHARIBIKA!! SERIKALI YAZID KUPOTEZA RASILIMALI ZAKE MUHIMU IKIWEMO GERAEZA LA MAGEREZA

Magari 18,pikipiki 7  Generator yateketezwa kwa moto.vyote vikiwa ni mali za halmashauri ya masasi na baadhi ni vya watumishi wa halmashauri hiyo. Gereza la Masasi liko hatarini kupoteza wafungwa wote kwa kuvunjwa na waandamanaji hao
 OFISI ZA ELIMU MASASI ZACHOMWA MOTO

 
 MAGARI YA HALMASHAURI NA WAFANYAKAZI WA HALMASHAURI YACHOMWA MOTO

 GENERATOR YA MANISPAA YACHOMWA MOTO

 AMBULANCE YA HALMASHAURI YACHOMWA MOTO
View detail

MASASI NAKO HAKUKALIKI, VURUGU KUBWA WANANCHI HAWATAKI GESI ITOKE. GARI NA NYUMBA YA MBUNGE NA MAHAKAMA YA MWANZO VYATEKETEA KWA MOTO

 Gari la maji yakuwasha lahisiwa halina maji, askari walipanda wakashuka kulikimbia
Habari nilizozipata hivi punde kutoka Masasi ni kuwa maandamano yameanza tena na safari hii yanaongozwa na dereva boda boda ambao wameingia barabarani.
Risasi za moto na mabomu ya machozi yanapigwa kutawanya watu na tayari nyumba moja imechomwa moto. Gari la maji ya kuwasha limefika ila bado watu wanazidi kuongezeka
Tayari gari na nyumba ya mbunge imechomwa moto na vijanga wanazidi kusonga mbele wakiwa na madumu ya petrol
Mahakama ya mwanzo imechomwa.moto na polisi wamejifungia ndani.wanarusha mabomu ya machozi wakiwa ndani. Askari magereza wamejaribu kuwasha gari la maji ya kuwasha lakini bahati mbaya halina.maji hivyo wakashuka na kukimbia na wananchi wanataka kulichoma moto
View detail

MTWARA HAKUKALIKI! NYUMBA YA HAWA GHASIA YACHOMWA MOTO, MWANDISHI WA CHANEL TEN AJERUHIWA. POLISI WA MTWARA WAZIDIWA. POLISI LINDI NA SONGEA WAENDA KUONGEZA NGUVU. SERIKALI IKO KIMYAA!!


Askari wa kutuliza ghasia wakijiandaa kuzuia vurugu zilizotokea Mtwara, leo kwa kile kilinachodaiwa ni mwendelezo wa vurugu za madai ya gesi.

 

Katika vurugu hizo, mwandishi wa habari wa Chanel Ten, amejeruhiwa kichwani na kukimbizwa hospitali kwa ajili ya kupatiwa matibabu, huku ikielezwa kuwa watu hao wamevamia Nyumba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu,Tawala na Serikali za Mitaa, Hawa Ghasia, na kuipiga mawe na kuvunjwa vioo na kuchomwa moto.
 
Aidha imeelezwa kua katika harakati hizo pia Mahakama ya Mwanzo imechomwa moto na kusababisha askari kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya watu hao na kulazimika Jeshi la Wananchi Tanzania JWTZ, kuingilia kati kutuliza ghasia hizo.
 
View detail

Thursday, January 24, 2013

KINONDONI WAPATIWA VIFAA VYA KUTUNZIA TAKA


002
Meneja Mikopo wa BankABC, Eugenia Shayo akikabidhi sehemu ya vifaa 100 vya kubebea taka kwa Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda vyenye thamani ya sh milioni 3.5.

003
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda akizungumza na waandishi wa habari, mara baada ya kukabidhiwa vifaa hivyo.
Manispaa ya Kinondoni imekabidhiwa vifaa 100 vya kutunzia taka na benki ya BankABC vyenye thamani ya shilingi milioni 3.5 leo Dar es Salaam. Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kupokea vifaa hivyo, Meya wa Manispaa hiyo, Yusuph Mwenda amesema Manispaa yake itahakikisha usafi unazingatiwa na mkazi atakayebainika kutupa taka ovyo atachukuliwa hatua kali ikiwemo kumtoza faini ya kuanzia shilingi 50,000 mpaka 10,000 “Hii ni kampeni maalumu
View detail

JK ATUA FIFA ZURICH

8E9U4801
FIFA President Joseph Sepp Blatter welcomes President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete to FIFA headquarters in Zurich,Switzerland this afternoon.President Kikwete was at  FIFA headquarters at the invitation of FIFA President Joseph Sepp Blatter.


8E9U4814
President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete, his host FIFA President Joseph Sepp Blatter and TFF President Leodegar Chilla Tenga pose at the entrance of FIFA Headquarters in Zurich,Switzerland this afternoon.
8E9U4849
FIFA President Joseph Sepp Blatter presents a souvenir FIFA flag to President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete this afternoon at  Mr. Blatter’ s office in Zurich this afternoon.
8E9U4859
President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete settles for conversation with FIFA President Sepp Blatter at his FIFA headquarters’ office in Zurich this afternoon.
8E9U4864
President Dr.Jakaya  Mrisho Kikwete in conversation with FIFA President Sepp Blatter at FIFA    Headquarters in Zurich this afternoon.
8E9U4870
FIFA president Joseph Sepp  Blatter shows President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete   various   World  trophies on display at FIFA headquarters in Zurich, Switzerland.
8E9U4886
FIFA president Joseph Sepp  Blatter shows President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete   various   World  trophies on display at FIFA headquarters in Zurich, Switzerland.
8E9U4888
FIFA President Joseph Sepp Blatter points to a football played during the last World cup tournament in South Africa while President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete looks on.
8E9U4899
President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete speaks to reporters soon after he visited FIFA headquarters in Zurich, Switzerland .Second left is FIFA President Joseph Sepp Blatter and on the right is TFF President Leodegar Chilla Tenga.
8E9U4920
President Dr.Jakaya Mrisho  Kikwete bids farewell to his host FIFA president Joseph Sepp Blatter after visiting FIFA headquarters in Zurich, Switzerland  at the invitation of Mr. Blatter(photos by Freddy Maro)
8E9U4979
FIFA President Joseph Sepp Blatter and TFF President Leodegar Chilla Tenga
View detail

HABARI MPASUKO: HALI SI SHWARI MSIMBATI MKOANI MTWARA

MKUU WA MKOA WA MTWARA (MH SIMBA KALIA)
Gari la usalama wa taifa pajero limebondwa mawe na kuchomwa moto msimbati usiku huu,inasadikika kijana mmoja jina kapuni mzaliwa wa msimbati kazi sikio alienda na gari msimbati na kumshawishi bibi mwenye msimbati asie taka gasi itoke na kumtaka kumchukua bibi kwendanae dar,ghafla akazingukwa na watu pale nyumbani wakaanza kumburuza akakimbilia kusiko julikana.baba wa huyu jamaa jina kapuni anaishi pale ligula polisi wamemwagwa kijijini Msimbati, wazee kadhaa wa kimila wamepigwa sana. 

View detail

Wednesday, January 23, 2013

Bi Clinton kujitetea kuhusu Benghazi


Bi Clinton alitarajiwa kuhojiwa mwaka jana lakini akaugua
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Hillary Clinton, anatarajiwa kufika mbele ya bunge la Congress kujieleza kuhusu mashambulizi mabaya yaliyofanywa dhidi ya ubalozi wa Marekani mjini Benghazi, Libya, mwaka jana.
Bi Clinton atakabiliwa na maswali kutoka kwa kamati za bunge la Senate na la waakilishi kuhusu maswala ya kigeni, juu ya usalama mbovu uliosababisha mashambulizi hayo.
Alitarajiwa kujieleza mbele ya kamati hiyo mwaka jana lakini akaugua.
Balozi wa Marekani nchini Libya Christopher Stevens pamoja na maafisa wengine watatu wa ubalozi huo, waliuawa kwenye mashambulizi hayo.
Balozi huyo alifariki kutokana na moshi wakati aliponaswa ndani ya jengo lililokuwa linateketea.
Hii ni baada ya wapiganaji wa kiisilamu kuvamia ubalozi.

Mashambulizi hayo yalisababisha mvutano wa kisiasa swali lilikuwa nani aliyekuwa na taarifa kuhusu shambulizi hilo.


Baada ya kushambulia ubalozi wavamizi walichoma bendera ya Marekani kuonyesha kero lao
Kutokana na hilo, jopo maalum lilbuniwa kuchunguza tukio hilo.
Kwa kuwa Clinton ni mwanachama wa Democrat ambao wanadhibiti bunge la Senate, atakuwa anahojiwa kwa njia ya heshima lakini atakabiliwa na wakati mgumu kutoka kwa wabunge wa bunge la waakilishi ambao wengi ni wanachama wa Republican.
Jopo hilo huenda lisimlimbikizie lawama sana Clinton kwa utovu wa usalama kwenye ubalozi huo, lakini wanachama wa Congress bado watataka kujua kwa nini hakuwa na taarifa kuhusu ombi la kuimarisha usalama katika ubalozi huo.
Pia atakabiliwa na maswali kuhusu ambavyo serikali ya Obama ilishughulikia mzozo huo.
Wafanyakazi watatu wa serikali walifutwa kazi kuhusiana na shambulizi la Benghazi na mapendekezo yaliyotolewa na jopo hilo mwezi Disemba tayari yanashughulikiwa.
View detail

Watu 5 wakatwa vichwa Maiduguri,Nigeria


Washukiwa wa kundi la kiisilamu wamewakata vichwa watu kadhaa mjini Maiduguri, Kaskazini mwa Nigeria.
Mtu mmoja ameambia azizicompdoc.blogspot.com  kuwa wanaume watano waliuawa wakati wa msako katika nyumba za watu usiku wa kuamkia leo.
Miongoni mwa walionyongwa ni baba na mwanawe.
Hata hivyo, jeshi la Nigerialimesema ni watu watatu pekee waliouawa.
Zaidi ya watu 20 sasa wamefariki katika mashambulizi tofauti, Kaskazini mwa Nigeria wiki hii pekee ambayo yanshukliwa kusababishwa na kundi la
Boko Haram pamoja na makundi mengine yanayotaka nchi hiyo kutumia sheria za kiisilamu.
Boko Haram wamelaumiwa kwa mauaji ya watu 23 katika mashambulizi tofauti Kaskazini mwa Nigeria.
Walio shuhudia mauaji hayo wanasema kuwa washambuliaji waliwalenga watu waliokuwa wanauza nyama ya wanyamapori, katika eneo la Damboa siku ya Jumatatu na kuwaua watu 18.
Watu wengine watano walifariki Jumanne wakati kundi la wanaume waliokuwa wanacheza mchezo wa kamari walishambuliwa mjini Kano.
Kundi la Boko Haram, linalopigana kutaka kuweka sheria za kiisilamu, nchini Nigeria limekuwa likifanya mashambulizi, katika sehemu kadhaa nchini humo.
Boko Haram imelaumiwa kwa vifo vya takriban watu 1,400, Kaskazini mwa Nigeria tangu mwaka 2010. Mwaka jana pekee , kundi hilo lilihusishwa na vifo vya watu 600.
Siku ya Jumatatu, watu waliokuwa wamejihami, walifyatulia risasi katika soko moja jimbo la Borno , wakiwalenga watu waliokuwa wanauza nyama ya nyani, na nguruwe.
Silaha zilizonaswa kutoka kwa kundi la Boko Haram

Waisilamu wengi hawatumii kabisa nyama ya wanyama pori.
"watu waliokuwa wamejihami, na wanaoshukiwa kuwa wanachama wa kundi la Boko Haram, walikuja katika soko moja eneo hilo, na kuwapiga risasi watu 13, papo hapo na wengine watano walifariki kutokana na majereha yao.'' alisema afisaa mmoja.
Eneo la Damboa liko karibu na hospitali moja mjini Borno katika jimbo la Maiduguri, ngome ya Boko Haram.Kundi hilo liliundwa mjini humo mwaka 2002.
Wakati huohuo, ripoti zinasema kuwa shambulizi lengine baya sana limefanywa mjini Kano , mji mkuu Kaskazini mwa Nigeria,umbali wa kilomita 500, Magharibi mwa Damboa.
Watu waliokuwa wanaendesha pikipiki waliwanywaftulia risasi, vijana waliokuwa wanacheza nje , kwa mujibu wa taarifa za polisi.
Mchezo wa kamari pia umeharamishwa katika dini ya kiisilamu.
View detail

RAIS KIKWETE AFUNGUA SHULE YA SEKONDARI YA MLIMANI MATEMWE ZANZIBAR

 


 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiangalia vitabu vya masomo katika maktaba ya shule mpya ya Sekondari ya Mlimani Matemwe muda mfupi baada ya kuifungua rasmi jana.Kulia ni Ofisa mwandamizi kutoka ofisi ya Benki ya Dunia nchini anayeshughulikia masuala ya elimu Bwana Nobuyuki Tanaka na kushoto ni Mwalimu mkuu wa Shule hiyo Mohamed Mzee Choum.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Iddi(kulia) na Afisa mwandamizi  kutoka katika kitengo cha elimu katika ofisi ya Benki ya Dunia nchini Bwana Nobuyuki Tanaka wakikata utepe wakati wa hafla ya ufunguzi wa Shule ya Sekondari ya Mlimani  Matemwe huko Zanzibar jana.Shule hiyo imejengwa kwa ushirikiano kati ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Benki ya Dunia. Picha na Freddy Maro wa Ikulu
View detail

CHUO KIKUU HURIA CHA TANZANIA (THE OPEN UNIVERSITY OF TANZANIA) CHAANZISHA KOZI MPYA!!KARIBU UELIMIKE!! USINGOJE KUSIMULIWA!!

23 wauawa kwenye mashambulizi Nigeria



Washukiwa wa kundi la wapiganaji wa kiisilamu , wamelaumiwa kwa mauaji ya watu 23 katika mashambulizi tofauti Kaskazini mwa Nigeria.
Walio shuhudia mauaji hayo wanasema kuwa washambuliaji waliwalenga watu waliokuwa wanauza nyama ya wanyamapori, katika eneo la Damboa siku ya Jumatatu na kuwaua watu 18.
Watu wengine watano walifariki Jumanne wakati kundi la wanaume waliokuwa wanacheza mchezo wa kamari walishambuliwa mjini Kano.
Kundi la Boko Haram, linalopigana kutaka kuweka sheria za kiisilamu, nchini Nigeria limekuwa likifanya mashambulizi, katika sehemu kadhaa nchini humo.
Boko Haram imelaumiwa kwa vifo vya takriban watu 1,400, Kaskazini mwa Nigeria tangu mwaka 2010. Mwaka jana pekee , kundi hilo lilihusishwa na vifo vya watu 600.
Siku ya Jumatatu, watu waliokuwa wamejihami, walifyatulia risasi katika soko moja jimbo la Borno , wakiwalenga watu waliokuwa wanauza nyama ya nyani, na nguruwe.
Silaha zilizonaswa kutoka kwa kundi la Boko Haram

Waisilamu wengi hawatumii kabisa nyama ya wanyama pori.
"watu waliokuwa wamejihami, na wanaoshukiwa kuwa wanachama wa kundi la Boko Haram, walikuja katika soko moja eneo hilo, na kuwapiga risasi watu 13, papo hapo na wengine watano walifariki kutokana na majereha yao.'' alisema afisaa mmoja.
Eneo la Damboa liko karibu na hospitali moja mjini Borno katika jimbo la Maiduguri, ngome ya Boko Haram.Kundi hilo liliundwa mjini humo mwaka 2002.
Wakati huohuo, ripoti zinasema kuwa shambulizi lengine baya sana limefanywa mjini Kano , mji mkuu Kaskazini mwa Nigeria,umbali wa kilomita 500, Magharibi mwa Damboa.
Watu waliokuwa wanaendesha pikipiki waliwanywaftulia risasi, vijana waliokuwa wanacheza nje , kwa mujibu wa taarifa za polisi.
Mchezo wa kamari pia umeharamishwa katika dini ya kiisilamu.
View detail

Tuesday, January 22, 2013

Ufaransa yazidiwa nchini Mali Uingereza yajitosa kuisaidia

Hali yawa tete kwa serikali ya Ufaransa nchini Mali. Serikali ya Uingereza inatarajiwa kujadili mpango wa kutoa msaada zaidi kwa wanajeshi wa Ufaransa wanaopambana na waasi nchini Mali.
Wanajeshi wa Mali wampokea msaada kutoka kwa Ufaransa na sasa Uingereza inataka pia kuwasaidia

Serikali ya Uingereza inatarajiwa kujadili mpango wa kutoa msaada zaidi kwa wanajeshi wa Ufaransa wanaopambana na waasi nchini Mali.
Waziri mkuu David Cameron, amesema kuwa huenda msaada za usafiri na kijasusi ukatolewa kwa wanajeshi hao. Ndege mbili za kijeshi tayari zimetolewa kwa jeshi la Ufaransa.
Waziri wa ulinzi anasema kuwa hakuna mipango ya kufanya mashambuli ya ardhini kwa sasa.
Kuhusu vifo vya raia wa Uingereza katika mashambulizi kwenye kiwanda cha gesi nchini Algeria yaliyofanywa na wapiganaji wa kiisilamu, bwana Cameron alisema kuwa eneo la Kaskazini mwa Afrika linageuka kuwa ngome ya wapiganaji wa kiisilamu.
Wasiwasi kuhusu athari za kundi la kigaidi la al-Qaeda katika ukanda huo, zinaonekana kudhibitiwa kufuatia mpango wa kuwapeleka wanajeshi wa Ufaransa kupambana na wapiganai wenye uhusiano na Al Qaeeda nchini Mali na Algeria ambako waliwateka nyara wafanyakazi wa kigeni.
Wanamgambo waliowashambulia wafanyakazi wa kigeni nchini Algeria, ambapo takriban mateka 48 waliuawa wametoa wito kwa Ufaransa kusitisha harakati zao nchini Mali.

Waiziri mkuu alisema kuwa Uingereza pamoja na washirika wake wako katika mapambano dhidi ya kasumba ambayo inatia doa kubwa dini ya kiisilamu na ambayo inaamini kuwa mauaji na ugaidi yanakubalika na tena ni sharti yafanyike.
Jibu la jamii ya kimataifa kwa tisho hili liitakuwa swala muhimu katika ajenda ya mkutano wa nchi nane zilizostawi duniani G8.
"lazima tupambane na hao magaidi kwa kutumia mbinu zote za kuweka usalama. Lazima tuwakomeshe, kijeshi. Ni lazima tuzungumzie hii kasumba yao, sharti tufunge hii nafasi wanayoitumia, kuendesha harakati,zao'' alisema waziri mkuu.
View detail

Why Shop on Bongo Online?

We make your shopping experience easy and exciting with our multiple payment options, amazing deals and unbeatable prices. You may pay on delivery or online with your Mobile Money. We fulfill your orders within the estimated time frame at your preferred location. We are committed to serving you, and your satisfaction is of utmost importance to us. Rest assured that for a wonderful shopping experience, Bongo Online Shop is the best place to be

About

Swissgear Smart Bag

468x60 Ads

HIDDEN CAMERA

Support : tzamaizing@gmail.com | Tzamaizing Template | +255 653 33 29 24
Copyright © 2015. AZIZI COMPUTER DOCTOR - All Rights Reserved
Template Created by Tzamaizing Published by Tzamaizing
Proudly powered by Bongo Online Shop